Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

05 Februari 2018

Wanasiasa, Wafanyabiashara na Watu Maarufu wafika Uhamiaji kujipatia pasipoti za kielektroniki

Baada ya Idara ya Uhamiaji kuanza rasmi kutoa pasipoti za kielektroniki, Baadhi ya Wafanyabiashara na wanasiasa wakubwa nchini wameanza kufika Makao Makuu ya Uhamiaji kupata pasipoti hizo. Miongoni mwa waliofika kujipatia pasipoti ni Wafanyabiashara maarufu nchini Mzee Reginald Mengi akiwa na mkewe pamoja na Mzee Said Salim Bakhresa. 

Kwa upande wa wanasiasa, Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Edward Lowassa alifungua pazia kwa wanasiasa waliofika Uhamiaji Makao makuu kujipatia pasipoti hizo za kisasa zenye usalama wa hali ya juu.

Akiongea mara baada ya kupatiwa pasipoti yake, Mzee Mengi alisema amefurahishwa na mabadiliko makubwa ya kiutendaji ambapo amefanya maombi na kupatiwa pasi ndani ya siku moja kitu ambacho awali hakikuwepo.

''Hii ni hatua kubwa sana kwa kweli, Uhamiaji mmejitahidi mno, mimi na mke wangu tumefanya maombi leo na kupata pasipoti zetu, hongereni sana kwa hili" alisema Mzee Mengi ambaye aliambatana na Mkewe Bi. Jacqueline.

Naye Mheshimiwa Lowassa alisifu juhudi zinazofanywa na Idara  ya Uhamiaji kwenye dhana ya Uhamiaji Mtandao ambapo ampongeza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala kwa juhudi zake za kuifanaya Idara ya Uhamiaji kwenda sambamba na tekinolojia.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni