Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

11 Machi 2021

Hivi ndivyo Wanawake Uhamiaji Zanzibar walivyowafariji watoto yatima katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani

Zanzibar

Katika shamra shamra za kuadhimisha siku ya wanawake duniani iliyofanyika tarehe 8 Machi ya kila mwaka wanawake wa uhamiaji kwa kushirikiana na wafanyakazi wote wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar walitoa misaada mbali mbali kwa watoto yatima ambao wanaishi katika mazingira magumu pamoja na kufanya usafi wa mazingira yanayozunguka kituo hicho.

Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Chiku Khamis Omar alikabidhi misaada katika kituo cha watoto yatima kiitwacho Markaz Alyaqiin Islamic Centre kilichopo Kinduni Mkoa wa Kaskazini  Unguja kwa niaba wanawake wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi misaada hiyo Kamishna Msaidizi Chiku amewashukuru viongozi wa watoto hao kwa kukubali kupokea misaada hiyo na kuwaahidi kua wanawake wa Uhamiaji wataendelea kutoa misaada zaidi kwa watoto hao kila hali itakaporuhusu.

Miongoni mwa misaada hiyo ni pamoja na mchele, sukari, sabuni, vitakasa mikono na mipira ya kuchezea.

Nae kiongozi wa kituo hicho Maalim Adam Bakar Haji ambae ni kaimu Mwenyekiti wa kituo hicho amewashukuru wanawake wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar kwa kuwapelekea watoto misaada hiyo na kuwaomba mashirikiano zaidi juu ya suala la kuwalea watoto hao.

 Aidha Watoto hao yatima wakiongozwa na mtoto Abdulrahman Aly Mussa walisoma dua maalum ya kuwaombea wanawake hao ikiwa ni shukran kwao.

Kwa upande wa Zanzibar Kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya wanawake duniani ni ‘’Badili fikra: imarisha ushiriki wa wanawake katika maamuzi kwa maendeleo endelevu’’.

HABARI PICHA NA MATUKIO


Vifaa mbali mbali vikitolewa na uhamiaji Zanzibar

(Maafisa Uhamiaji Zanzibar wakishiriki kufanya usafi)




(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Zanzibar)



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni