Matangazo

📢 IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA — KARIBU KWENYE BLOG RASMI   ✦   📰 UHAMIAJI HABARI BLOGU — TUNAKULETEA MATUKIO KILA SIKU   ✦   📲 FUATA IDARA YETU KATIKA MITANDAO YA KIJAMII   ✦   ✉️ WASILIANA NASI: info@immigration.go.tz   ✦   ☎️ +255-22-2850575/6

07 Oktoba 2019

“IMARISHENI MAPAMBANO DHIDI YA WAHAMIAJI HARAMU NCHINI”- Dkt. Makakala













Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala leo Jumatatu Oktoba 7, 2019 amewataka Maafisa Uhamiaji Mikoa yote nchini kuimarisha Mapambano dhidi ya Wahamiaji haramu.

Akizungumza na Watumishi wa Uhamiaji Mkoa wa Rukwa (mjini Sumbawanga), Dkt. Makakala amesema kuwa nchi yetu inaelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na baadae Uchaguzi Mkuu. Hivyo Maafisa Uhamiaji Mikoa yote nchini wametakiwa kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo kwa kutoa Elimu kwa umma pamoja na kuhakikisha kuwa Wahamiaji haramu hawashiriki zoezi hilo.

Kwa ushirikiano na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Idara ya Uhamiaji inatarajia kutoa Elimu ya Uraia kwa kuanzia na Mikoa ya Kagera, Kigoma, Rukwa, Katavi na Geita. Maafisa Uhamiaji wote nchini wametakiwa kuandaa vipindi maalum vyenye lengo la kuwajengea uwezo na uzalendo wananchi hususan katika masuala ya Uraia.

“Kila Mwananchi anao wajibu wa kulinda usalama wa nchi yetu kwa kutoa taarifa za Wahamiaji haramu. Kumhifadhi au kumsaidia Mhamiaji haramu kupata kitambulisho cha mpiga kura na kushiriki zoezi la kupiga kura kwa ama kuchagua au kuchaguliwa ni kukosa uzalendo kwa nchi yetu” amesisitiza Dkt. Makakala.

“Taifa lolote Duniani liwe kubwa au dogo haliwezi kukamilika bila ya raia wake kwani raia hao ndio wenye nchi na wanaotakiwa kunufaika na haki zitolewazo na serikali kwa raia wake kwa mujibu wa katiba ya nchi ikiwa ni pamoja na haki ya kuchagua au kuchaguliwa katika nafasi za uongozi Kwa upande mwingine ni raia hao ndio wenye wajibu wa kulinda nchi yao” aliongeza Dkt. Makakala.

Awali akitoa taarifa ya Utendaji kazi katika Mkoa wa Rukwa, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Rukwa, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Elizeus Mshongi ameeleza kuwa mkoa wa Rukwa unapokea idadi kubwa ya wahamiaji haramu, wengi wao wanatoka katika Mataifa ya Zambia, D.R Congo na Burundi.

Kwa kipindi cha cha kuanzia Januari hadi Agosti, 2019; jumla ya wahamiaji haramu 128 wamekamatwa na kuchukuliwa hatua mbalimbali ikiwamo kushitakiwa na kuondoshwa nchini.

Naibu Kamishna Mshongi ameongeza kuwa Mkoa unaendesha zoezi la kuwatambua na kuwaorodhesha Wahamiaji walowezi. Kupitia Zoezi hilo jumla ya Walowezi 5,743 wametambuliwa na kuorodheshwa.

Aidha, Idara ya Uhamiaji inatoa wito kwa Wahamiaji walowezi wote wanaoishi nchini kujitokeza na kujiorodhesha, watakaoshindwa kufanya hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani na kuondoshwa nchini.


“Tumejipanga kutoa huduma bora”, KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akiongea na Watumishi katika Kituo cha Uhamiaji Tunduma mwishoni mwa wiki.

Kamishna wa Udhibiti na Usimamizi wa Mipaka, Kamishna wa Uhamiaji Samwel Mahirane akitoa taarifa ya utendaji kazi wa kituo cha Uhamiaji Tunduma kwa waheshimiwa Marais wa Tanzania na Zambia mra baada ya uzinduzi wa kituo cha huduma ya pamoja mpakani (OSBP) katika mpaka wa Tunduma.














Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala amewaagiza Watumishi wa Idara ya Uhamiaji kufanya kazi kwa weledi na kujiepusha na vitendo vya rushwa wakati wanapotoa huduma kwa Wananchi na raia wa kigeni.

Dkt. Makakala  ametoa wito huo ikiwa ni Utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoyatoa wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Kituo cha Pamoja cha Huduma Mpakani (One Stop Border Post - OSBP) cha Tunduma - Nakonde, tarehe Oktoba 5, 2019.

Awali Kamishna Jenerali alipokea taarifa ya utendaji kazi wa kituo hicho na amewataka kuimarisha doria maeneo ya mipakani na kushirikiana na watendaji kata na vijiji katika kuwabaini wahamiaji haramu wanaojipenyeza na kuishi katika maeneo yao.

Idara ya Uhamiaji kama mdau wa huduma mapakani hapo imeshiriki hafla uzinduzi wa Kituo hicho (Tunduma – Nakonde OSBP) uliofanywa kwa pamoja na Marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Jamhuri ya Zambia, Mhe. Edger Lungu.  

Idara ya Uhamiaji imejipanga kutoa huduma bora na za kisasa mpakani hapo kwa kutumia mfumo wa Uhamiaji Mtandao (e-immigration) ambapo Vifaa vya kisasa vimefungwa ili kufanikisha upatikanaji wa huduma bora za Kiuhamiaji. 

Mfumo huu pia utawezesha kudhibiti mpaka huo kwa njia ya kielektroniki (e-Border Management Systems) suala ambalo litasaidia ulinzi na usalama.
Mfumo huu (e-Immigration) utatatua kero zinazosababishwa na urasimu usio wa lazima katika utoaji wa huduma za kiuhamiaji.













05 Oktoba 2019

“FANYENI KAZI KWA WELEDI NA KUZINGATIA SHERIA”, DKT. MAKAKALA


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala ametoa rai hiyo alipokuwa akizungumza na Watumishi wa Idara ya Uhamiaji katika Mkoa wa Mbeya.

Akizungumza na Watumishi hao, Kamishna Jenerali amewasihi kujiepusha na vitendo vya rushwa na kufanya kazi kwa weledi na bidiii ili kwenda sambamba na kasi ya serikali ya Awamu ya Tano katika kuwaletea wananchi wake maendeleo na kukuza uchumi wa nchi yetu.

“Idara ya Uhamiaji ina jukumu kubwa la kukuza sekta za Utalii na Uwekezaji katika nchi yetu hivyo tunatakiwa kuwahudumia wageni wanaoingia na kuishi nchini bila vikwazo vinavyoweza kurudisha nyuma ustawi wa sekta hizo” amesitiza Dkt. Makakala.

Kwa upande wake Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Shaaban Omari ameeleza kuwa Idara inaendelea na mapambano dhidi ya Wahamiaji kwa kuwashirikisha Viongozi wa Serikali za Mitaa na Kata.

Viongozi hao Kata na Vijiji wanapatiwa Elimu ya Uhamiaji ili kuwajengea uelewa katika masuala ya Kiuhamiaji ikiwa ni maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kutekeleza Mpango Mkakati wa Mapambano dhidi ya Wahamiaji haramu (Pekenyua Fukunyua) unaondelea nchi nzima kwa sasa.

Akiwa katika ziara hiyo Mkoani Mbeya, Dkt. Makakala ametembelea na kukagua Ofisi za Uhamiaji katika Vituo vya Uwanja wa Ndege wa Songwe pamoja na Mpaka wa Kasumulu.

Kesho Jumamosi Oktoba 5, 2019, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji atahudhuria Uzinduzi wa Kituo cha pamoja cha utoaji huduma za mpakani (OSBP) katika Mpaka wa Tunduma Mkoani Songwe ambapo mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akisalimiana na Maafisa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Uhamiaji Mkoa huo siku ya Alhamisi tarehe 04 Oktoba 2019 katika ziara ya kikazi mkoani humo.


Kaimu Mfawidhi wa kituo cha Uhamiaji Kasumulo akimuonesha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji eneo litakalojengwa kityoo cha Mpaka wa Pamoja (OSBP).


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akiongea na raia wa DRC Bwana Jeane Pierre aliyekuwa akipata huduma za Uhamiaji katika mpaka wa Tunduma

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji pamoja na Kamishna wa Udhibiti na Usimamizi wa Mipaka wakiangalia ukamilishaji wa maandalizi ya ufunguzi wa kituo cha huduma za pamoja mpakani (OSBP) katika mpaka wa Tanzania na Zambia mji mdogo wa Tunduma. 

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akisaini kitabu cha wageni katika kituo cha Uhamiaji Tunduma mkoani Songwe



28 Septemba 2019

NAIBU KATIBU MKUU RAMADHAN KAILIMA ATEMBELEA OFISI YA UHAMIAJI MAKAO MAKUU

Naibu Katibu Mkuu Ramadhani Kailima na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala wakifurahia jambo na wananchi ambao wapo kwenye foleni ya kusubiria huduma ya kupewa pasipoti kwa dharura.

Mkuu wa Kitengo cha Tehama Kamishna Msaidizi Mwandamizi Mohamed Awesu akimwonyesha Naibu Katibu Mkuu namna mfumo wa Tehama wa e-Immigration unavyofanya kazi nchi nzima


Naibu Katibu Mkuu Ramadhani Kailima akiangalia pasipoti ya kieletroniki baada ya kuchapishwa alipotembelea chumba cha Passport Printing, Uhaimiaji Makao Makuu.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima akingalia jinsi pasipoti inavyokaguliwa katika mfumo kwenye hatua ya mwisho kabla ya kutolewa ili itumike

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Ramadhani Kailima
ametembelea Ofisi ya Uhamiaji Makao Makuu Dar es Salaam na kujionea namna  Idara hiyo ilivyojipanga kuwahudumia Wananchi.


 Akiwa Ofisini hapo, Naibu Katibu Mkuu huyo alipata fursa ya kukagua Mfumo wa utoaji wa huduma ya Pasipoti.


 Maeneo aliyotembelea na kukagua ni Kaunta ya kupokelea maombi, Chumba maalum cha kuchukulia alama za vidole kielektroniki, Ofisi ya Uhakiki na Udhinishaji wa maombi hayo pamoja na Ofisi ya Uchapishaji wa Pasipoti (Passports' Printing Room).
 Naibu Katibu Mkuu huyo pia amekagua Kitengo cha Utoaji wa Pasipoti kwa haraka/dharura kwa Wananchi wenye mahitaji maalum.


 Kabla ya kuhitimisha Ziara yake, Naibu Katibu Mkuu Kailima alipata fursa ya kuzungumza na Wananchi na raia wa kigeni walifika Ofisini hapo kwa ajili ya kupatiwa huduma mbalimbali za kiuhamiaji.


 Aidha, Naibu Katibu Mkuu Kailima amemuagiza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala kuanzisha utoaji wa huduma za Pasipoti kwa haraka (express).
 "Nimelezwa kuwa kwa sasa Waombaji wa Pasipoti wanapatiwa kwa muda siku  ..., Hivyo  anzisheni Mfumo wa utoaji wa Pasipoti kwa haraka (express) na Wananchi watakao hitaji huduma hiyo wachangie kiasi kidogo cha fedha na kupatiwa Pasipoti zao kwa muda wa siku moja", alizungumza Kailima.


 Aliongeza kuwa wapo baadhi ya Wananchi hawapendi kutumia muda wao mwingi kwenye foleni wakati wanaweza kulipia kiasi kidogo cha fedha ili kupata huduma kwa haraka.
  Kwa upande wake Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala
alimwahidi Naibu Katibu Mkuu huyo kutekeleza maelekezo aliyoyatoa katika ziara hiyo.
 Dkt. Makakala ameongeza kuwa Idara ya Uhamiaji imejiimarisha vyema kutekeleza Mradi wa Uhamiaji Mtandao kwa lengo la kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi na wageni.
 Kupitia Mfumo huo, Jumla ya Pasipoti 187,787 na hati za dharura za safari (Emergency Traveling Documents - ETDs) 255,534 zimetolewa kwa Watanzania.


 Dkt. Makakala ameongeza kuwa Idara ya Uhamiaji inatekeleza vyema dhana kuimarisha sekta za Utalii na Uwekezaji Nchini. Kupitia Mfumo huu, Idara imetoa Vibali vya Ukaazi 6,848 kwa Wageni waliongia na kuishi Nchini kwa madhumuni mbalimbali ikiwemo Uwekezaji.
  Pia Idara ya Uhamiaji imetoa viza 152,377 kwa Wageni walioingia nchini kwa madhumuni mbalimbali ikiwemo Utalii na Matembezi.


 Mfumo wa Uhamiaji Mtandao unaohusisha Utoaji wa huduma za kielektroniki za Pasipoti, Viza, Vibali vya Ukaazi pamoja na Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka umezinduliwa mnao Januari 31, 2018 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.


19 Septemba 2019

WAHITIMU UHAMIAJI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUZINGATIA SHERIA






Wahitimu wa mafunzo ya Uongozi ya Maafisa Uhamiaji wametakiwa kutumia elimu waliyoipata  kufanya kazi kwa bidii, weledi na kwa kuzingatia sheria ili kuboresha huduma za kiuhamiaji  kwa wageni na wananchi kwa ujumla.

Hayo yamezungumzwa na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala wakati akifunga Mafunzo ya Maafisa Uhamiaji Daraja la Pili yaliyofanyika katika Chuo cha Magereza cha Gereza Kuu Kingolwira - Morogoro mwanzoni mwa wiki hii. 
Dkt. Makakala amewataka wahitimu hao kuzingatia dhana ya uwajibikaji hivyo kutumia elimu waliyoipata kupitia mafunzo hayo kufanya kazi kwa uadilifu na bidii ili kuboresha huduma kwa wageni na raia wa Tanzania.

“Mafunzo mliyopata yawe chachu na kuongeza hamasa katika kutoa huduma iliyotukuka kwa wageni na kuifanya Tanzania kuwa sehemu salama ya uwekezaji bila kuweka vikwazo zinavyo kwamisha uwekezaji nchini”, alisisitiza Dkt. Makakala. 

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Magereza cha Gereza Kuu Kingolwira - Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Lazaro Nyanga (ACP) amewapongeza wahitimu hao kwa kuonesha nidhamu kwa kipindi chote cha mafunzo na amewata kuendeleza uadilifu huo watakapokuwa kwenye vituo vyao vya kazi.

“Wamekuwa wakijitolea na kufanya kazi kwa bidii na kushiriki katika shughuli za kijamii na wakati mwingine kujitolea kutatua changamoto mbalimbali zinazokikabili chuo chetu ikiwa ni pamoja na kutumia nguvu kazi kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya chuo chetu. Hivyo naomba nichukue fursa hii kuwashukuru, kuwapongeza na kuwataka waendelee kuwa na moyo huo kwa wakati wote watakapokuwa kazini ili kuchangia jitihada za Serikali kwa mambo mbalimbali katika sehemu zao za kazi”, aliongeza Kamishna Msaidizi wa Magereza Nyanga.

Akizungumza na Uhamiaji Media Mmoja wa Wahitimu hao Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Vedasto Rwekiza Venant amesema kuwa mafunzo hayo yamekuwa chachu kwao na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote waliyopewa na Viongozi wakati wa kufunga mafunzo hayo.

Ikumbukwe kwamba Mafunzo haya yanafanyika kutokana na Marekebisho ya Sheria ya Uhamiaji Na. 8 ya Mwaka 2015 (The Immigration Ammendment Act, 2015).

Kupitia marekebisho hayo yameiingiza Idara ya Uhamiaji katika Tume ya Polisi, Uhamiaji na Magereza hatua ambayo kimsingi yamechangia uwepo wa mabadiliko katika kuajiri, upandishwaji wa vyeo, utoaji wa stahili na mafunzo mbalimbali.

Tayari Idara ya Uhamiaji imetoa mafunzo kwa Maafisa na Askari 642 hadi sasa, kwa kozi maalum za kijeshi za kupandishwa vyeo (Promotion Course) katika Shule ya Polisi Moshi na Chuo cha Magereza cha Gereza Kuu Kingolwira - Morogoro. Awamu ya kwanza kwa kipindi cha Mwezi Aprili na Juni 2017, jumla ya Maafisa na Askari 222 wamehitimu. Awamu ya Pili imehusisha Maafisa na Askari 362 kwa mafunzo yaliyofanyika kati ya Mwezi Februari na Julai, 2018. 

Sherehe hizo za ufungaji wa mafunzo hayo zimehudhuliwa na Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu (CI-Znz), Kamishna wa Uhamiaji, Utawala na Fedha Edward Peter Chogero (CI-A&F), Kamishna wa TRITA, Maurice Kitinusa (CI-TRITA), Kamaishna wa Magereza, Huduma za Urekebishaji, Tusikile Mwaisabela (CP), Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa Morogoro, Wananchi wa Morogoro, Waaalikwa pamoja na na Waandishi wa habari.



16 Septemba 2019

DKT MAKAKALA KUFUNGA MAFUNZO YA UONGOZI YA MAAFISA UHAMIAJI



Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala kesho Jumanne tarehe 17 Septemba, 2019 anatarajia kufunga Mafunzo ya Uongozi ya awamu ya nne kwa Maafisa 54 wa ngazi ya Wakaguzi Wasaidizi wa Uhamiaji ambao wamehitimu mafunzo hayo.


Akitoa taarifa hiyo Mjini Morogoro, Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Mrakibu Mwandamizi Alhaji Ally Mtanda amesema kuwa Mafunzo hayo yatafungwa na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala katika Chuo cha Magereza cha Gereza Kuu Kingolwira – Morogoro.


Sherehe hizo za ufungaji wa mafunzo hayo zitahudhuriwa na Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu  (CI-Znz), Kamishna wa Uhamiaji,  Utawala na Fedha Edward Peter Chogero (CI - A&F), Kamishna wa TRITA, Maurice Kitinusa  (CI - TRITA), Afisa Uhamiaji Mkoa Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Angela Mathew Shija (ACI) pamoja na Wakuu wa  Vitengo mbalimbali kutoka Ofisi ya Uhamiaji Makao Makuu.