Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

09 Aprili 2020

Muendelezo wa Ziara ya Utambulisho wa Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji katika kituo cha Azam TV

Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano Mrakibu wa Uhamiaji, Paul John Mselle mapema wiki hii ameendelea na ziara ya utambulisho katika vyombo mbalimbali vya habari.

Ambapo wiki hii ametambulishwa rasmi katika studio za Azam TV na U FM zilizopo Tabata Jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Uhai Productions na Watangazaji wa Habari wa Azam TV na U fm Redio.

Tukio hilo liliratibiwa na aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Mrakibu Mwandamizi, Alhaj Ally Mohamed Mtanda ambaye amehamishiwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kuongozwa Bi. Timzo Kalugira mtangazaji wa Azam. 

HABARI PICHA NA MATUKIO
Mkurugenzi wa Habari Azam Tv Bi. Jane Shirima (katikati) akiwapokea Msemaji Mkuu wa Uhamiaji Tanzani na Aliyekuwa Msemaji wakati wa ziara ya Utambulisho katika studio za Azam Tv mapema wiki hii
 



Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Tanzania na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano Mrakibu wa Uhamiaji, Paul John Mselle (Kulia) akifanya mazungumzo na Mtangazaji wa Azam Tv Baraka Mpenja 
Bi. Timzo Kalugira Mtangazaji wa Azam Tv wa kwanza (kushoto) akitoa maelezo juu ya utayarishaji na uandaaji wa vipindi unavyofanyika katika studio za Azam Tv


Baadhi ya Waandishi wa Habari wa Azam Tv Wakiwa katika Majukumu yao ya Kawaida


 

Ndani ya Studio za 107.3 U fm Dar es salaam

(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni