Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

13 Aprili 2020

Uhamiaji Mkoa wa Mara yapokea Kontena kutoka Barrick North Mara

Mara, Tanzania
Katika kuendeleza jitihada za kuunga mkono serikali katika ulinzi na usalama hapa nchini Mgodi wa Barrick North Mara Mkoani Mara umetoa kontena moja (tupu) kwa Idara ya Uhamiaji   wilayani Butiama Mkoani Mara litakalotumika kama Ofisi ndogo katika Kizuizi cha Kirumi ikiwa na lengo la kurahisisha utendaji kazi katika kizuizi hicho.

Akiongea wakati akipokea kontena hilo Afisa uhamiaji Mkoa wa Mara Naibu Kamishna wa Uhamiaji DCI Albert Rwelamila aliwapongeza wakurugenzi wa Barrick North Mara kwa kutoa kontena hilo kwani litasaidia  katika utendaji kazi wa kawaida na kufanya doria za ulinzi imara katika Mipaka ya nchi ili kuendelea kudumisha hali ya amani na usalama wa wananchi na mali zao .

Awali Kizuizi hicho hakikuwa na ofisi au sehemu ya Kutosha  kujikinga na jua au mvua kwa askari wakati wa utekelezaji wa majukmu yao, hivyo kontena hilo limefika wakati muafaka hasa katika kipindi hiki cha kupambana na wahamiaji haramu wanaojaribu kujipenyeza kuingia nchini bila kufuata utaratibu kutokana na ugonjwa wa COVID -19 Unaosababishwa na virusi vya Corona.

Aidha DCI Rwelamila akiwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Tarime na Rorya ACP William Mkondya waliweza kuongea na askari waliopo katika kizuizi hicho cha Kirumi kwenye barabara ya Sirari-Musoma- Mwanza, walipofanya ziara ya kukagua utendaji kazi katika vituo mbalimbali vya mipaka na vizuizi Mkoani Mara.

Katika ziara hiyo  walitoa  wito na maelekezo kwa Maafisa na askari wa vituo hivyo juu ya  kushirikiana kwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama katika udhibiti wa uingiaji wa wageni nchini kinyume na sheria hasa wakati huu wa juhudi za kupambana na kudhibiti kuenea kwa maambuki ya virusi vya Corona.


HABARI PICHA NA MATUKIO
DCI Albert Rwelamila Afisa Uhamiaji Mkoa Mara (aliyevaa Barakoa Kulia) akikagua utendaji kazi wa madaktari wanaopima abiria katika kizuizi cha Kirumi  juu ya maambukizi ya covid 19 Kabla ya Kukutana na Huduma za Kiuhamiaji

 DCI Albert Rwelamila Afisa Uhamiaji Mkoa Mara akiwa na Kamanda Kanda Maalumu ACP William Mkondya wakiongea na askari katika kizuizi cha Kirumi kwenye barabara ya Sirari-Musoma- Mwanza 


Picha ya Pamoja DCI Rwelamila, (Katikati waliosimama) kushoto kwake ni ACI Othuman Makame, Mrakibu Msaidizi Adam Tebuye akifuatiwa na Mhasibu David Sanga, Kulia kwa DCI Rwelamila  ni Maafisa Uhamiaji na Waliochuchumaa ni Wadau walioleta kontena kutoka - Barrick North Mara

Afisa Uhamiaji Mkoa aliyevaa T-shirt nyeupe akitoa maelekezo kwa Maafisa wa Uhamiaji juu ya matumizi ya kontena lililopokelewa katika kizuizi cha Kirumi (Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Mkoa wa Mara). 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni