Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

08 Oktoba 2020

CGI Dkt. Anna Makakala Ahudhuria Hafla ya Uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis Dar es salaam.

Dar es salaam

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini (CGI) Dkt. Anna Makakala Mapema leo hii  amehudhuria Hafla ya Uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis Jijini Dar es salaam 

Hafla hiyo iliongozwa na Rais wa Malawi Dkt. Lazarus Chakwera na Mwenyeji wake Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .

Aidha tukio hilo limehudhuriwa pia na Wakuu wengine wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama sanjari na Mawaziri mbalimbali Makatibu wakuu wa wizara na Viongozi wengine waandamizi wa serikali bila kuwasahau wananchi wa Jiji la Dar es salaam na Tanzania kwa Ujumla

Kituo hicho cha Mabasi Kitagharimu Zaidi ya Bilioni 70 za Kitanzania ambazo ni fedha za ndani, huku lengo kuu likiwa ni kuwahudumia Wananchi wa Tanzania na Wageni wengine kutoka Nchi Mbalimbali za Jirani na zile za SADC.

HABARI PICHA NA MATUKIO

Muonekano wa Ujenzi wa Kituo Kipya cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis Jijini Dar es salaam Ukiendelea

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Akiongea na Wananchi wa Dar es salaam wakati wa Ufunguzi wa Kituo cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis Dar es salaam

Rais wa Malawi Dkt. Lazarus Chakwera akiongea na Wananchi wa Dar es salaam wakati wa Uuwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis Dar es salaam

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini (CGI) Dkt. Anna Makakala akipokea maelezo ya namna Kituo cha Mabasi Kitakavyokuwa  baada ya kuhudhuria Hafla ya Uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis Jijini Dar es salaam 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Seleman Jaffo akitoa Maelezo ya Mradi wa Ujenzi wa Kituo Kipya cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis


Muonekano wa Jengo la Kituo cha Mabasi Mbezi Luis Ujenzi Ukiendelea






Baadhi ya Makatibu Wakuu wa Wizara Waliohudhuria Hafla hiyo


Baadhi ya Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama waliohudhuria Hafla hiyo





Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini (CGI) Dkt. Anna Makakala akimuaga Rais wa Malawi Dkt. Lazarus Chakwera (Hayupo Pichani) baada ya kumaliza tukio la  Hafla ya Uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis Dar es salaam.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini (CGI) Dkt. Anna Makakala akimuaga Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli baada ya kumaliza tukio la  Hafla ya Uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kituo cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis Dar es salaam.



Kamishna wa Jeshi la Magereza Nchini (CGP) Suleiman Mzee akiagana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli baada ya  Ufunguzi wa Kituo cha Kisasa cha Mabasi Mbezi Luis Dar es salaa

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi  Dkt. John Kijazi  (Kulia) akiteta Jambo na Mkuu wa Itifaki (Chief of Protocol)  Balozi Kanali Wilbert Ibunge baada ya Kuhitimisha Hafla ya Uwekaji Jiwe la Msingi katika  Kituo Kipya cha Mabasi Mbezi Luis Dar es salaam 


(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni