Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

10 Novemba 2020

UHAMIAJI IIringa yakamata Wahamiaji Haramu Raia wa Somalia

Iringa, Tanzania

Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Iringa mapema wiki hii imekamata wahamiaji Haramu wanne 04 raia wa Somalia na Dereva mmoja (01) raia wa Tanzania wakati wa doria ya kawaida.

Akithibitisha Taarifa hizo Afisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji (SACI) Agnes Michael Luziga amesema watuhumiwa wote walikamatwa eneo la Mazombe Wilayani Kilolo na Kikosi Maalumu cha doria cha Askari wa Uhamiaji Mkoa wa Iringa wakati wakitekeleza majukumu yao ya kila siku.

Baada ya mahojiano imebainika kuwa watuhumiwa walikuwa wakitokea Mkoani Dar es salaam kama abiria kwenye gari namba T592 DTY aina ya Hiace wakielekea Mkoani Mbeya na baadae Afrika ya Kusini kupitia Malawi, Aliongeza (SACI) Luziga.

Kwa Mjibu wa sheria za Uhamiaji Sura namba 54, Rejeo la Mwaka 2016 pamoja na kanuni zake, Watuhumiwa wote watafikishwa Mahakamani kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha Sheria na kusafirisha wahamiaji haramu,

Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Iringa inaendelea kutoa wito kwa jamii kuendelea kutoa ushirikiano pindi wanapo mtilia shaka mtu yoyote  ili kuwezesha kudhibiti uingiaji na utokaji wa watu kupitia utekelezaji wa sheria na kanuni zilizopo ili kulinda usalama wa Taifa  na kukuza maendeleo ya Kiuchumi.

HABARI PICHA NA MATUKIO
Watuhumiwa Walioingia Nchini Kinyume cha Sheria 

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACI) Agnes Michael Luziga




Gari iliyotumika Kusafirishia Wahamiaji Haramu (Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Mkoa wa Iringa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni