Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

25 Novemba 2020

Uhamiaji Kagera yatoa Elimu kwa Umma katika Uzinduzi wa Wiki ya Huduma za Sheria.

Kagera

Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kagera mapema wiki hii imeshiriki katika uzinduzi wa Wiki ya Huduma za Sheria nchini inayoendelea Mkoani humo Wilayani Karagwe katika Viwanja vya stendi ya Omurushaka villivyopo kata ya Bugene.

Uzinduzi huo uliongozwa  rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti, huku Idara ya Uhamiaji ikitumia wiki hiyo kutoa Elimu kwa Umma kuhusu masuala ya Uraia,  taratibu za Kupata Pasipoti  na kuelimisha wananchi kuhusu madhara ya Wahamiaji haramu kuingia nchini ambapo ni hatari kwa ulinzi na Usalama wa Taifa letu.

#Wananchi Fichueni Wahamiaji Haramu

#Jukumu la Ulinzi na Usalama wa Taifa letu ni la kila Mtanzania

 HABARI PICHA NA MATUKIO


Mkuu wa Mkoa Kagera Brigedia Marco Gaguti Akiongea na wananchi wa Karagwe hawapo Pichani Wakati wa Ufunguzi wa Wiki ya Huduma za Sheria

Baadhi ya Maafisa Uhamiaji Mkoa wa Kagera wakihudumia Wananchi wa Karagwe

Kazi Inaendelea

(Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Kagera)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni