Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

01 Desemba 2020

Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Azindua Jengo la Afisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kaskazini Unguja

Zanzibar 

Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar (CI) Johar M. Sururu mapema wiki hii amezindua Jengo la Afisi ya Uhamiaji iliyoko Mkoa wa Kaskazini Unguja baada ya kampuni ya Albatna Building Contractors co. LTD kukamilisha Ukarabati wake.


Akiongea na Maafisa, Askari na Watumishi raia wakati wa makabidhiano hayo Kamishna Sururu ametoa maelekezo ya kuhakikisha Majengo hayo yanatunzwa, yanathaminiwa na yanawekewa mazingira mazuri kwa manufaa ya Kizazi cha sasa na baadae.

Aidha amesisitiza kuzingatia umuhimu wa upatikanaji wa majengo mapya uende sambamba na utoaji wa huduma bora zenye kiwango cha kitaifa na Kimataifa sanjari na kuwataka kufanya kazi kwa Utii, Uhodari na Weledi wa hali ya juu.

“Tunataka huduma zetu ziendane na Jengo hili jipya na sitarajii kusikia malalamiko kutoka kwa wananchi “Alisema

Kwa upande wake Mhandisi wa Kampuni Albatna Building Contractors Co. ltd Bwana Seif M. Said alisema, ukarabati huo umefanyika kwa kuzingatia muda ulioweka pamoja na vigezo vyote villivyohitajika ili jengo liweze kudumu kwa muda mrefu.

Idara ya Uhamiaji Tanzania imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa manufaa ya Idara na Taifa kwa ujumla, hali inayopelekea kuimarisha haiba ya usalama wa majengo na kukuza uchumi wa Taifa.

 HABARI PICHA NA MATUKIO

Makabidhiano


Muonekano wa Jengo la Afisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kaskazini Unguja baada ya Kukarabatiwa (Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Zanzibar)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni