Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

23 Desemba 2020

CGI Dkt. Anna Makakala awataka SUMAJKT Kuongeza Kasi ya Ujenzi Makao Makuu ya Uhamiaji Dodoma

Dodoma

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini Dkt. Anna Makakala mapema wiki hii amefanya ziara katika eneo la Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji, Jijini Dodoma na Kutoa Maelekezo kwa Kampuni ya Ujenzi ya SUMAJKT Kuongeza kasi ya Ujenzi ili kumaliza Jengo hilo mapema iwezekanavyo. 

CGI Dkt. Makakala amemtaka Mkandarasi wa Mradi huo kufanya kazi Usiku na Mchana ili jengo hilo liweze kukamilika kwa haraka.

Hata hivyo Dkt. Makakala ametoa pongezi kwa Mkandarasi huyo kwa kujenga jengo lenye ubora litakalochangia katika kuboresha huduma bora za Ki-Uhamiaji zinazokidhi viwango vya Kitaifa na Kimataifa.

Jengo hilo lenye ghorofa 08 litakapokamilika linaweza kuwa la kwanza kwa Ukubwa  hapa Jijini Dodoma.

HABARI PICHA NA MATUKIO

Muonekano wa Maendeleo ya Ujenzi wa Jengo Jipya la Idara ya Uhamiaji Makao Makuu ya Nchi Dodoma
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini Dkt. Anna Makakala akisaini Kitabu cha wageni





Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini Dkt. Anna Makakala akiangalia Ubora wa baadhi ya milango  itakayotumika katika eneo la Basement





Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini Dkt. Anna Makakala akiendelea na Ukaguzi


Mafundi kutoka Kampuni ya Ujenzi ya SUMAJKT Wakiendelea na kazi ya kumwaga nzege katika Jengo Jipya la Makao Makuu ya Uhamiaji Jijini Dodoma



Kazi Inaendelea





Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini Dkt. Anna Makakala akiangalia baadhi ya vifaa vinavyotumika kufanyia kazi.








Kazi ya Nzege ikiendelea


(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni