Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

16 Desemba 2020

Waziri Simbachawene Atoa Maagizo Mazito kwa SUMAJKT Kumaliza Ujenzi Makao Makuu ya Uhamiaji Dodoma

Dodoma

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene, mapema wiki hii amefanya ziara katika eneo la Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji, Jijini Dodoma na Kutoa Maelekezo kwa Kampuni ya Ujenzi ya SUMAJKT Kufanya kazi masaa 24. 

Mhe. Simbachawene amemtaka Mkandarasi wa Mradi huo kuongeza kasi ya Ujenzi kwa kufanya kazi Usiku na Mchana ili jengo hilo liweze kukamilika kwa haraka.

Amesema jengo hilo la ghorofa nane lilipaswa kukamilika mwezi Disemba, 2020, lakini mpaka sasa lipo asilimia 41 jambo ambalo hajaridhishwa nalo. 

Hata hivyo Mhe. Simbachawene alitoa pongezi kwa Mkandarasi huyo kwa kujenga jengo lenye ubora mkubwa litakalochangia katika kuboresha huduma bora za Ki-Uhamiaji zinazokidhi viwango vya Kitaifa na Kimataifa.

 "Jengo hili litakapokamilika linaweza kuwa la kwanza hapa Dodoma kwa ukubwa, hivyo nawataka Wajenzi hawa kuongeza kasi ili tuweze kuhamia hapa mapema iwezekanavyo," alisema Mhe. Simbachawene.

Idara ya Uhamiaji Inaendelea kutekeleza majukumu yake mbalimbali ikiwemo Kudhibiti uingiaji na utokaji wa watu kupitia utekelezaji wa sheria na kanuni zilizopo ili kulinda Usalama wa Taifa na kukuza maendeleo ya Kichumi huku ikiongozwa na Kauli mbiu ya Uhamiaji, “Usalama na Maendeleo”

MATUKIO KATIKA PICHA

Muonekano wa Ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji Tanzania linaloendelea kujengwa Jijini  Dodoma


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene akisalimiana na Konstebo wa Uhamiaji  Innocent Swallo  Kutoka Kitengo cha Majengo Uhamiaji Makao Makuu 

Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji  (ACI)Joseph Mtenga Akisikiliza wa Makini Maelekezo ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi alipofika kufanya Ziara ya Kukagua Maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji Jijini Dodoma

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene akisaini kitabu cha wageni



Ukaguzi Ukiendelea







Ujenzi Ukiendelea






Ukaguzi Ukiendelea


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene akiongea na Waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza Ukaguzi wa maendeleo ya Ujenzi (Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni