Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

22 Desemba 2020

UHAMIAJI Kilimanjaro yashiriki mazishi ya SI Anna Mushi

Kilimanjaro

Maafisa na askari wa Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro wakiongozwa na Afisa Uhamiaji Mkoa Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Edward Mwenda wameshiriki katika mazishi ya aliyekuwa Mrakibu wa Uhamiaji Anna Mushi yaliyofanyika Marangu Mkoani Kilimanjaro.

Akiwasilisha salamu za rambirambi kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala, Afisa Uhamiaji Mkoa ACI Mwenda ameeleza namna marehemu alivyokuwa tunu kwa Idara ya Uhamiaji na serikali kwa ujumla.

Katika muda wote aliofanya kazi marehemu alikuwa na utii uhodari na weledi wa hali ya juu, hivyo ameondoka Idara ikiwa bado inamhitaji.

Marehemu Mrakibu Anna Moshi alikuwa akifanya kazi katika Kituo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl JK. Nyerere (JNIA) Jijini Dar es salaam na amefariki hivi karibuni baada ya kuugua muda mrefu.

ACI Mwenda amewaomba ndugu, jamaa na marafiki kuwa wavumilivu ktk kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao.

#Bwana alitoa bwana ametwaa Jina la bwana lihimidiwe

HABARI PICHA NA MATUKIO

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji (ACI) Edward Mwenda akitoa salamu za mwisho




(Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji (M) Kilimanjaro)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni