Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

23 Desemba 2020

Uhamiaji FC Yaanza Ligi Daraja La Kwanza kwa Kishindo

Zanzibar

Timu ya mpira wa miguu ya Uhamiaji Zanzibar mapema wiki hii imeanza vyema katika mechi zinazoendelea kuchezwa Visiwani humo, ikiwa ni mechi za ligi daraja la kwanza kanda ya Unguja.

Timu hiyo imeibuka kidedea kwa kupata ushindi wa goli 2-1 dhidi ya mpinzani wake Mchangani United iliyojinyakulia bao moja katika dakika ya 56 katika mechi iliyochezwa katika viwanja vya Mau.

Mabao hayo  kwa upande wa Uhamiaji FC yamefungwa na mchezaji Kassim Ramadhan katika dakika ya 12 na Haji Khamis Mnachia katika dakika ya 46 na kupelekea ushindi huo.

HABARI PICHA NA MATUKIO

Kikosi cha Timu ya Uhamiaji Zanzibar

(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Afisi Kuu Zanzibar)


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni