Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

28 Desemba 2020

Uhamiaji Mbeya yatoa msaada katika kituo cha watoto yatima.

Mbeya

Katika kuelekea Mwishoni mwa mwaka 2020 na kuukaribisha mwaka 2021 Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mbeya imetumia fursa hiyo kutoa msaada kwa watoto yatima ikiwa ni njia mojawapo ya wajibu wa kijamii yaani (Corporate Social Responsibility)

Shughuli hiyo imeongozwa na Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACI) Msafiri Shomari akishirikiana na Maofisa na Askari wa Uhamiaji wa Mkoa huo katika, kituo cha watoto  yatima kiitwacho MKATE WA WATOTO YATIMA Kilichopo  Iwambi Jijini Mbeya ambacho kina jumla ya watoto 30.

Baadhi ya mahitaji muhimu yaliyotolewa na Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mbeya ni kama vile mchele,mafuta,sabuni ,sukari nk.

SACI Shomari alieleza kwamba pamoja na msaada huo kwa kituo hicho bado kina uhitaji mkubwa kwa ajili ya ustawi wake na maendeleo mazuri ya watoto, huku akiwaomba wadau wengine kujitokeza na kuweza kusaidia watoto wenye uhitaji.

HABARI PICHA NA MATUKIO




(Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji (M) Mbeya)
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni