Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

10 Novemba 2017

IDARA YA UHAMIAJI YAPOKEA UJUMBE 'MZITO' KUTOKA JUMUIYA ZA KIMATAIFA

Idara ya Uhamiaji imepokea ujumbe wa Maafisa kumi na tisa (19) toka nchini Ivory Coast na Niger. Maafisa hao ambao ni viongozi waandamizi wa Serikali, Shirika la Uhamiaji la Kimataifa (IOM), Mashirika ya Kimataifa ya Kikanda ya AU, UEMOA na ECOWAS walifanya ziara ili kubadilishana uzoefu wa utendaji kazi baina ya mataifa hayo ya Afrika Magharibi na Tanzania.

Mwenyeji wao Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Kamishna Hannelore Manyanga alipokea ujumbe huo katika Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es Salaam, ambapo baada ya kusalimiana na kuingia ukumbi wa mikutano,  wajumbe hao walipata maelezo mbalimbali ya Huduma zinazotolewa na Idara ya Uhamiaji. 

Pia wajumbe hao walipata fursa ya kujifunza kuhusu taratibu za Uingiaji na Utokaji nchini, mifumo ya utambuzi na taarifa za wasafiri pamoja na masuala ya udhibiti na usimamizi wa mipaka.

Kiongozi wa ujumbe huo Bwana Ouba Ibrahim kutoka nchini Niger alimshukuru Kaimu Kamishna Jenerali kwa mapokezi mazuri na mkutano uliokuwa na lengo la kubadilishana uzoefu wa utendaji kazi kati ya Uhamiaji Tanzania na idara za uhamiaji, polisi na forodha  za nchi za Niger na Ivory Coast. 



Afisa TEHAMA, Sajini  wa Uhamiaji,Philip Masilingi  akiwasilisha andiko kuhusu Utendaji wa Mfumo wa kutambua na kuhifadhi taarifa za wasafiri mbele ya wajumbe wa Shirika la Uhamiaji wa Kimataifa, IOM kutoka nchi za Ivory Coast na Niger. Wajumbe hao ni pamoja na Maafisa Uhamiaji, Polisi na Forodha. 

Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Godbless Swai akiwasilisha andiko kuhusu taratibu za uingiaji  na ukaazi nchini na kwa jumbe huo. 

Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Omary Othman akiwasilisha andiko kuhusu udhibiti na usimamizi wa miopaka nchini kwa jumbe huo. 
Afisa kutoka Shirika la IOM nchini Bwana Marcellino Ramkishun akichangia mada katika Kikao cha Idara ya Uhamiaji na Ujumbe uliongozwa na Shirika lake.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Kamishna Hannelore Morgan Manyanga mwenye Uniform katika akiwa katika picha ya pamoja na wageni wa IOM waliotembembelea Makao ya Makuu ya Uhamiaji kwa ziara ya Mafunzo


Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Kamishna Hannelore Morgan Manyanga akiagana na Ouba Ibrahim kutoka Niger ambaye ni mmoja wa wajumbe waliotembembelea Makao ya Makuu ya Uhamiaji kwa ziara ya Mafunzo, kuria kwake ni Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Mrakibu Ally Mohamed Mtanda  


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni