Matangazo

📢 IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA — KARIBU KWENYE BLOG RASMI   ✦   📰 UHAMIAJI HABARI BLOGU — TUNAKULETEA MATUKIO KILA SIKU   ✦   📲 FUATA IDARA YETU KATIKA MITANDAO YA KIJAMII   ✦   ✉️ WASILIANA NASI: info@immigration.go.tz   ✦   ☎️ +255-22-2850575/6

03 Novemba 2017

JUMLA YA MAAFISA UHAMIAJI 15 WAAGWA LEO KUELEKEA CHINA

Jumla ya Maafisa Uhamiaji 15 wameagwa leo jijini Dar es salaam tayari kwa safari kuelekea nchini China kwa ajili ya mafunzo ya wiki mbili.

Hafla hiyo fupi iliyofanyika Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini wilaya ya Temeke iliwakutanisha maafisa uhamiaji kutoa maeneo mbalimbali nchini ambao wanasafiri mwisho wa wiki hii.

Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Hannelore Manyanga aliwatakia safari njema maafisa hao na kuwasisitiza kuzingatia mafunzo watakayopewa ili waje kutumia ujuzi watakaoupata kwa ajili ya maendeleo ya Idara.


Maafisa hao wanategemea kuondoka nchini mwishoni mwa wiki kuelekea jijini ShangChuan. 



Maafisa Uhamiaji wanaosafiri mwishoni mwa wiki kuelekea nchini China wakiwa katika picha ya pamoja

Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Hannelore Manyanga (aliyekaa) katika picha ya pamoja na 'wasafiri'

Kiongozi wa Msafara, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Mariam Mwanzalima akitoa neno la shukrani kwa niaba ya 'wasafiri'

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni