Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

24 Novemba 2017

ZIARA YA KAMISHNA WA UHAMIAJI VIZA NA PASI KATIKA MIKOA YA DODOMA, IRINGA NA NJOMBE KATIKA PICHA


Kamishna wa Uhamiaji Viza na Pasi, Mwichum  Salum  amefanya ziara katika Mikoa ya Dodoma,Iringa na Njombe kuongea na Maafisa na askari wa Uhamiaji kupanga mikakati ili kuzidisha utendaji wa kazi wa idara,aidha Kamishna Mwichum ametembela vituo vya wilayani kujionea hali halisi ya utendaji kazi. 
Kamishna wa Uhamaiji Viza na Pasi Mwichum H Salum  akisikiliza taarifa ya utendaji kazi  kutoka kwa Afisa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma Naibu Kamishna wa Uhamiaji Peter Jerome Kundy

Kaimishna wa Uhamiaji Viza na Pasi Mwichum Salum akimsikiliza Afisa uhamiaji mkoa wa Njombe  Kamishna msaidizi Hosseh Kagimbo kwenye kituo cha Makambako

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma Naibu Kamishna wa Uhamiaji Peter Jerome Kundy akisoma taarifa ya utendaji kazi kwenye kikao pamoja na wafanyakazi wa mkoa wa Dodoma.
Kamishna wa Uhamiaji Viza na Pasi Mwichum  Salum wa pili kutoka kushoto akiwa na Afisa Uhamiaji mkoa wa Njombe  Kamishna Msaidizi  Hosseh Kagimbo wa kwanza kutoka kushoto na msaidizi wake pamoja na Maafisa wa kituo cha Makambako
Maafisa wa Uhamiaji Mkoa wa Njombe wakiwa katika picha ya pamoja na Kamishna wa Uhamiaji Viza na Pasi baada ya kikao alichokifanya wakati wa ziara yake Mkoani hapo.
Kamishna wa Uhamiaji Viza na Pasi Mwichum Salum akiwa katika picha ya pamoja na maafisa na askari wa Mkoa wa Dodoma baada ya kikao.

Kamishna wa Uhamiaji Visa na Pasi Mwichum Saluh akipata maelezo kutoka kwa Afisa Uhamiaji Mkoa wa Njombe kwenye eneo ambalo ofisi ya Uhamiaji Mkoa 
itajengwa hapo baada ya Halmashauri kutenga maeneo ambayo ofisi zote za umma zitajengwa eneno hilo. 




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni