Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

22 Novemba 2017

WALIOKWENDA CHINA WAREJEA SALAMA NCHINI

Maafisa Uhamiaji 15 waliokwenda nchini China kwenye ziara ya mafunzo ya wiki mbili wamerejea nchini jana usiku wakitokea katika jiji la ShangChuan ambapo walipokelewa na Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji Ignasio Gunda Mgana.


Msafara huo ulifika Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar leo majira ya saa tatu asubuhi na kulakiwa na Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Hannelore Manyanga ambaye alipokea taarifa ya safari na mafunzo.
Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Mariam Mwanzalima ambaye ndiye kiongozi wa msafara huo alieleza namna walivyosafiri na kupokelewa na uongozi wa chuo cha Uhamiaji jimbo la ShangChuan na mafunzo waliyopata.

“Tunamshukuru Mwenyeezi Mungu kutuwezesha kwenda na kurudi salama, Afande naomba ufahamu kuwa wale wenzetu wa China walitupokea na kutukirimu sana. Mafunzo tuliyopata ndani ya wiki mbili hizo ni masuala ya Human trafficking, border management issues, smuggling, cybercrime, customer care na travel documents verification. Kwa kweli tumejifunza mambo mengi ambayo yametufungua na yatatusaidia sana katika utendaji kazi wetu wa kila siku, asante afande kwa kutuchagua kuiwakilisha idara katika mafunzo haya’’ alieleza Mwanzalima.

Naye Kaimu Kamishna wa Jenerali wa Uhamiaji Hannelore Manyanga aliwataka maafisa hao kutumia ujuzi waliopata katika mafunzo hayo ili kuboresha huduma za uhamiaji  na kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi wanaofika kwenye ofisi za uhamiaji.



Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Mariam Mwanzalima akimweleza Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Hannelore Manyanga juu ya safari yao ya China na Mafunzo waliyopata.


Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji Ignas Gunda Mgana (kushoto) akisikiliza kwa makini taarifa ya safari ya maafisa walikwenda nchini kwenye mafunzo ya wiki mbili

Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Mariam Mwanzalima akitoa taarifa ya safari ya mafunzo nchini China

Kaimu Kamishna wa Uhamiaji Hannelore Manyanga akipokea zawadi ya Ngao ya Urafiki na Ushirikiano baina ya  Tanzania na Idara ya Uhamiaji na Polisi ya China


Picha ya pamoja wa maafisa walio rejea kutoka nchini China na Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji (aliyekaa).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni