Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

30 Novemba 2017

Watumishi wa Kada ya Kiraia wa Uhamiaji wafanya Mkutano wa kutathmini utendaji kazi wa Idara kwa mwaka 2017

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Maj. Gen. Projest Rwegasira aliwaasa Watumishi wa Idara ya Uhamiaji kufanya kazi kwa weledi na nidhamu.

Akizungumza na Watumishi hao kwenye Mkutano huo uliofanyika jana TRITA Moshi Katibu Mkuu aliongeza kuwa Viongozi wa Idara ya Uhamiaji na Watumishi wengine watumie Mkutano huo kutathmini mafanikio na changamoto mbalimbali zinazokwamisha utendaji kazi wa Idara.

"Natambua kuwa vikao vya aina hii vipo kwa mujibu wa Sheria, lakini pia ni muhimu sana kwa watumishi wa Kada ya kiraia ambao wanafanya kazi katika Vyombo ambavyo mfumo wake wa uendeshaji ni wa kijeshi zaidi wakapata fursa ya kusikilizwa hoja zao, kwani ipo dhana miongoni mwa watumishi raia kuwa hawapati fursa ya kushiriki na kufahamu baadhi ya mambo muhimu yanayohusu maslahi yao katika Vyombo hivyo. Mimi naamini Baraza hili ni uwanja mzuri sana na uliowazi katika kujadili masuala mbalimbali yanayo gusa maslahi ya mtumishi pamoja na mwajiri wake mahala Pa Kazi. Hivyo muutumie vizuri uwanja huu kwa maslahi ya pande zote mbili" alisema Katibu Mkuu.

Hili ni Baraza kubwa la Kitaifa la Watumishi wa Idara ya Uhamiaji Tanzania TUGHE ambalo hufanyika kila mwaka likiwa na lengo la kutathmini utendaji kazi na kushughulikia maslahi ya Watumishi wa Kada ya Kiraia.

Mkutano huo ulihudhuriwa na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji (Mwenyekiti), Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar (Makamu Mwenyekiti), Makamishna wa Uhamiaji wa Divisheni za Fedha na Utawala, Pasipoti na Uraia, Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka, Viza na Pasi, Vibali vya Ukaazi na Wafawidhi wa Vitengo toka Uhamiaji Makao Makuu na Zanzibar.

Kadhalika Viongozi wa TUGHE tawi la Uhamiaji Bw. Shaame A. Hamad (Mwenyekiti), Triphonia J. Kimaro (Katibu), Eng. Amani Msuya (Naibu Katibu TUGHE - Taifa), Bi. Magreth Ngomuo (Katibu Baraza) na Naibu Katibu Baraza Bw. Tale Ndonje ni miongoni mwa viongozi  ambao walifanikisha na kuhudhuria Mkutano huo.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Maj. Gen. Projest Rwegasira akiwasili katika Chuo Cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA).

Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar akiwasili katika Chuo cha Uhamiaji Cha Kikanda (TRITA) kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akiwaongoza Makamishna wengine kumpokea Mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Mambo ya Ndani ya Nchi



Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Idara ya Uhamiaji Dkt. Anna P. Makakala akimuongoza Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Maj. Gen. Projest Rwegasira kuingia kwenye ukumbi wa mkutano



Wajumbe wakiwasili kwenye ukumbi wa mkutano




Mkuu wa Chuo cha Uhamiaji TRITA Commandant Maurice Kitinusa akiwakaribisha wajumbe















Viongozi wa Baraza wakiwaongoza wajumbe kuimba wimbo wa Watumishi 'Solidarity forever'










Hakuna maoni:

Chapisha Maoni