Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

22 Novemba 2017

KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI ATEMBELEA VITUO VYA MPAKANI MKOA WA MARA


Kamishina Jenerali wa Uhamiaji Dr. Anna P. Makakala leo tarehe 21 Novemba 2017 amefanya zaiara ya kikazi na kukagua Ofisi na Vituo vya Uhamiaji Mbalimbali Mkaoni Mara.  Ofisi alizotembelea ni Shirati na Vituo vya Mipakani wa Sirari (Mpaka wa Tanzania na Kenya)  na Shirati katika Ziwa Victoria, mpaka ambao unaunganisha nchi za Tanzania, Kenya na Uganda.

"Mkoa wa Mara umebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi ikiwemo ziwa Victoria ambalo limekuwa ni kivutio kwa wahamiaji haramu kutoka nchi jirani kuja na kufanya shughuli za uvuvi bila kufuata Sheria za nchi. Ni jukumu la kila Mwananchi kuwa mlinzi wa rasilimali za Taifa na kuhakikisha kuwa zinatumika kwa manufaa ya raia wa Tanzania na sio kwa wageni hususani wahamiaji haramu" alisema Kamishna Jenerali.


Katika ziara hiyo wilayani Rorya, Kamishna Jenerali aliyefuatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Hamad Masauni na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Malima walitembelea kituo cha uhamiaji Shirati na kukagua mpaka wa Tanzania  na Uganda katika ziwa Victoria. Pia alipata fursa ya kuongea na wananchi katika kijiji cha Nyang'ombe kilichopo mwambao mwa ziwa Victoria katika Wilaya ya Rorya na kuwaasa kushirikiana na Idara yake katika suala zima la ulinzi wa mpaka huo na kuwasisitiza kutowahifadhi wahamu haramu.




Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akifafanua jambo kwa wananchi katka mpaka wa Sirari
Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Malima akiwahutubia wanachi katika mpaka wa Sirari





Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akisikiliza kero za mwananchi akiwa na  Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Hamad Masauni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Malima katika mpaka wa Sirai.

Kutoka kuusho, Mkuu wa Mkoa Mara, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji wakikagua mpaka wa majini baina ya Tanzania na Kenya katika ziwa Victoria.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni