Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

20 Novemba 2017

UHAMIAJI YAFUNGA 'MITAMBO' YA UTAMBUZI KATIKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MWALIMU JULIUS NYERERE


Idara ya Uhamiaji katika Kituo cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) imefunga Vifaa vyenye mfumo mpya wa utambuzi na ulinganisho wa sura (Facial Recognition and Matching System) kwa abiria wanaoingia nchini.

Akiongea baada ya kupokea vifaa hivyo, Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Divisheni ya Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka Samwel Rhobby Magweiga, amesema kuwa huo ni muendelezo wa mikakati ya Idara katika kuimarisha na kuhuisha KANZIDATA ya wanaoingia nchini.

“Vifaa na mfumo huu utasaidia sana katika kukusanya taarifa za abiria wote wanaoingia nchini kupitia hapa (JNIA), kama mlivyofahamishwa, mfumo huu unachukua sura ya mtu na kulinganisha na sura nyingine zilizomo kwenye kanzidata ili kuhakikisha taarifa zilizo kwenye pasipoti yake ni za pekee na hakuna mtu mwenye sura kama yake au mtu mwenye sura ingine kuwa na taarifa kama zake.”Alieleza Kamishna Samwel Magweiga.

Awali wakati akabidhiana vifaa hivyo, Mwakilishi mkazi wa Shirika la Uhamiaji la Kimataifa (IOM) Dr. Qasim Sufi alisema kwamba IOM itashirikiana na Idara ya Uhamiaji katika suala zima la udhibiti wa uingiaji na utokaji wa raia na wageni.

Idara ya Uhamiaji kwa kushirikiana na shirika hilo, wamefunga vifaa vingine vyenye mfumo huo kwenye vituo vya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) pamoja na mpaka wa Holili kwa pande zote mbili za Tanzania na Kenya.

Kupitia ushirikiano huo na IOM, Idara ya Uhamiaji itaendelea kuimarisha maeneo yote ya mipaka kwa kufunga vifaa na mfumo huu wa kisasa zaidi kutumiwa hapa Afrika Mashariki.

Dr. Qasim Sufi Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji akifanyiwa majaribio katika mfumo wa utambuzi wa sura (Facial Recognition and matching system) katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam

Kamishna wa Uhamiaji (Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka) Samwl Magweiga (wa kwanza kulia) akisikiliza kwa makini namna mfumo huo unavyofanya kazi wakati wa ufungaji wa vifaa vyenye mfumo huo.


Nelson Gonzales (aliyeshika pasipoti) akielezea namna mfumo huo unavyofanya kazi Kamishna na Maafisa Uhamiaji wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere.







Kamishna Wa Uhamiaji (Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka) akieleza kuridhishwa na namna vifaa na mfumo huo unavyofanya kazi ya utambuzi na ulinganishi wa sura na taarifa za abiria wanaoingia nchini



Kamishna wa Uhamiaji (Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka) akikabidhiwa nyaraka za mfumo huo na Mwakilishi Mkazi wa IOM Dr. Qasim Sufi mara baada ya ufungaji wa vifaa hivyo.


Maoni 1 :

  1. That's where we want to be. Security is our first priority to our Nation. Tanzania Kwanza.

    JibuFuta