Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

05 Julai 2020

Mkuu wa Utawala na Fedha Uhamiaji Zanzibar atembelea Banda la Uhamiaji na Kupongeza kwa Maandalizi Mazuri

Dar es salaam, Tanzania
Mkuu wa Utawala na Fedha kutoka Idara ya Uhamiaji Zanzibar Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACI) Gharib Saleh Suleiman, ameipongeza idara ya  Uhamiaji Tanzania kwa kuendelea kutoa huduma bora za kiuhamiaji.

Ameyasema hayo mapema leo hii alipofanya ziara ya kutembelea Maonesho ya saba saba na kufurahishwa na namna idara ilivyojipanga kuwahudumia raia wa Tanzania na wageni mbalimbali waliotembelea banda hilo.

Baadhi ya Huduma zinaotolewa katika maonesho hayo ni pamoja na Elimu kwa ujumla juu ya huduma za Kiuhamiaji, ikiwemo Pasipoti, Uraia, visa, vibali vya Ukaazi, Udhibiti wa Mipaka nk.

Aidha SACI Suleiman alipata pia wasaa wa kutembelea mabanda mengine ya Maonesho yakiwemo ya JKT, Wizara ya Uvuvi, Mabanda ya Wajasiriamali kutoka, Zanzibar na Banda la Karume.

Maonesho haya ya 44 ya Biashara ya (DIFT) 2020 yalifunguliwa rasmi hapo jana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Katika Viwanja vya Saba Saba Vilivyopo Wilaya ya Temeke Jijini Dar es saalam.

HABARI PICHA NA MATUKIO


Mkuu wa Utawala na Fedha kutoka Idara ya Uhamiaji Zanzibar Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACI) Gharib Saleh Suleiman alipotembelea banda la Uhamiaji katika Maonesho ya Saba saba




Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Tanzania Mrakibu Paul Mselle akitoa Maelezo ya jumla Kwa Mkuu wa Utawala na Fedha kutoka Idara ya Uhamiaji Zanzibar Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACI) Gharib Saleh Suleiman



















(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni