Matangazo

📢 IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA — KARIBU KWENYE BLOG RASMI   ✦   📰 UHAMIAJI HABARI BLOGU — TUNAKULETEA MATUKIO KILA SIKU   ✦   📲 FUATA IDARA YETU KATIKA MITANDAO YA KIJAMII   ✦   ✉️ WASILIANA NASI: info@immigration.go.tz   ✦   ☎️ +255-22-2850575/6

21 Julai 2020

UHAMIAJI Tanzania Yapokea Vifaa kutoka IOM


Dodoma, Tanzania
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala amelishukuru Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) Tanzania kwa kuchangia vifaa mbali mbali vitakavyosaidia katika kuimarisha usimamizi na Udhibiti wa Mipaka nchini.

Ameyasema hayo jana Jijini Dodoma katika Ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji Tanzania baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo kutoka kwa Kiongozi wa shirika hilo hapa nchini (IOM-Tanzania Chief of Mission) Dr. Qasim Sufi.

Vifaa vilivyotolewa ni Pikipiki 5 aina ya Honda XL125, Darubini 6 (6 pairs of High Magnification Infrared Binoculars), Mifuko 8 ya Kambi (8 Camping Tents), Boksi 18 za vifaa vya kutolea Msaada wa huduma ya kwanza na Tochi 18.

HABARI PICHA NA MATUKIO
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala Akiwa ameshika moja ya kifaa kilichotolewa na IOM (Kulia) ni  Kiongozi wa shirika hilo hapa nchini (IOM-Tanzania Chief of Mission) Dr. Qasim Sufi.



Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala (Kushoto)Akiwa kwenye moja ya pikipiki iliyotolewa na IOM (Kulia) ni  Kiongozi wa shirika hilo hapa nchini (IOM-Tanzania Chief of Mission) Dr. Qasim Sufi.(Picha kwa hisani ya IOMTanzania)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni