Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

26 Agosti 2020

CGI Dkt. Anna Makakala Akagua Mpaka wa Holili (OSBP) na Kusisitiza Ushirikiano katika Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Nchi.

Rombo, Kilimanjaro

Kamishna Jenerali wa Idara ya Uhamiaji (CGI) Dkt. Anna Makakala amefanya ziara ya kikazi katika mpaka wa Holili OSBP unaotenganisha nchi ya Kenya na Tanzania Uliopo katika Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro ili kukagua hali ya ulinzi na usalama wa mipaka na utendaji kazi wa maofisa na Askari wa Uhamiaji hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani.

Akiongea na Maofisa, Askari na Watumishi mbalimbali wa Taasisi nyingine za serikali zilizopo katika mpaka huo amewataka kuendeleza ushirikiano uliopo na kuwa na umoja ili kufanikisha ulinzi na usalama wa mpaka kwa manufaa ya maendeleo ya Taifa na kizazi cha sasa na baadae.

Mpaka haulindwi na mtu mmoja unalindwa kwa ushirikiano na kufanya kazi kwa pamoja, kwani kufanya hivyo ndio nguzo kubwa  na muhimu ya kufikia mafanikio yetu kama nchi, pia tuendelee kukemea rushwa na kutojihusisha nayo kabisa kwani Rushwa ni Adui wa haki na inaweza kuliangamiza Taifa” Alisema CGI Dkt. Makakala

Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu CGI Dkt. Anna Makakala ametoa rai kwa wananchi wote wanaoishi mipakani kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kutoa taarifa pale wanapoona wageni wasiowatambua sanjari na kuwa walinzi namba moja kwani jukumu la ulinzi na usalama wa nchi ni jukumu letu sote.

Kwa upande wake Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACI) Tununasya Ng’ondya amemuomba Kamishna Jenerali wa Uhamiaji kuweza kuanzishwa kwa Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Rombo ili kusaidiana na Vituo vya Uhamiaji vya Holili na Tarakea kuweza kudhibiti wahamiaji haramu na kusogeza zaidi huduma nyingine za Kiuhamiaji karibu na wanachi zaidi

Akitoa taarifa ya hali ya Mpaka  Mfawidhi wa Kituo cha Uhamiaji Holili (OSBP)Mrakibu Michael Mtuba amesema hali ya ulinzi na usalama mpakani hapo ni shwari na wamejipanga vilivyo kuendelea kutimiza majukumu yao kwa uhodari na weledi wa hali ya juu huku wakishirikiana kwa karibu sana na taasisi zote zinazofanya kazi katika mpaka huo.

Ziara ya CGI Dkt. Anna Makakala ilianzia katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Rombo ambapo alikutana na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya na kufanya nayo mazungumzo juu ya namna ya kuendelea kulinda mipaka ya nchi yetu na kutokomeza kabisa uingiaji wa wahamiaji haramu katika vipenyo mbalimbali vilivyopo katika Wilaya hiyo ya Rombo.

HABARI PICHA NA MATUKIO

Kamishna Jenerali wa Idara ya Uhamiaji (CGI) Dkt. Anna Makakala akiongea na baadhi ya Maafisa, Askari na Watumishi wengine wa Taasisi zilizopo  katika mpaka wa Holili OSBP unaotenganisha nchi ya Kenya na Tanzania
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji (CGI) Dkt. Anna Makakala akisalimiana na Watumishi wa TRA alipofanya ziara ya kikazi katika mpaka wa Holili OSBP hivi Karibuni
Baadhi ya  Maofisa na Askari wa Uhamiaji wa Kituo cha Holili


Baadhi ya Maofisa wa Taasisi Mbalimbali zilizopo katika Kituo cha Holili OSBP Wakimsikiliza kwa Makini Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala alipofanya ziara mpakani hapo hivi karibuni

Kamishna Jenerali wa Idara ya Uhamiaji (CGI) Dkt. Anna Makakala akisaini kitabu cha wageni katika Kituo cha Uhamiaji Holili OSBP

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Naibu Kamishna Abdallah Towo akimsikiliza kwa Makini CGI Dkt. Anna Makakala wakati wa Kikao na Maofisa na Askari katika Kituo cha Uhamiaji Holili


Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACI) Tununasya Ng'ondya



Muonekano wa Jengo la Holili OSBP


Kamishna Jenerali wa Idara ya Uhamiaji (CGI) Dkt. Anna Makakala akiwa katika Picha ya Pamoja





Kamishna Jenerali wa Uhamiaji (CGI) Dkt. Anna Makakala akisalimiana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Rombo 

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji (CGI) Dkt. Anna Makakala akiwa katika Picha ya Pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Rombo (Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni