Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

24 Agosti 2020

CGI Dkt. Anna Makakala Aipongeza Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Mwanga.

Mwanga, Kilimanjaro

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala ameipongeza Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya Mwanga Mkoani Kilimanjaro inayoongozwa na Mkuu wa Wilaya Mhe. Thomas Cornel Apson kwa juhudi na mpango mkakati walionao wa kutokomeza wahamiaji haramu wilayani humo.

Ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua hali ya mipaka na utendaji kazi kwa maofisa na askari wa Uhamiaji nchini.

Akiwa katika ukaguzi wa kipenyo cha Kitobo, Kitoghoto na Mkisha Wilayani Mwanga CGI Dkt. Anna Makakala amefurahishwa na juhudi ambazo zinafanywa na Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro na Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Mwanga kwani wamehamasisha ulinzi shirikishi wa mipaka katika maeneo hayo kwa kushirikiana na wananchi na wadau Mbalimbali.

Aidha amelishukuru Shirika la Msalaba Mwekundu nchini (Red Cross) Mkoa wa Kilimanjaro kwa kusaidia kutoa baadhi ya vifaa vya kusaidia ulinzi katika vipenyo vya Kighoto ambapo wametoa Mahema (Tents) 02 ambayo hutumika na askari wa Uhamiaji na askari wa Jeshi la Akiba (Mgambo) wanaojitolea kulinda baadhi ya maeneo korofi yanayosadikika kupitisha wahamiaji haramu katika Wilaya hiyo sanjari na kutoa jozi 02 za sare za Askari wa Jeshi la Akiba.

Mkuu wa Wilaya Mwanga Mhe. Thomas Apson Akiongea na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini CGI Dkt. Anna Makakala ofsini kwake amempongeza kwa utendaji kazi wake na uhodari katika kuiongoza vyema Idara ya Uhamiaji Kwa mafanikio makubwa.

Mhe. Apson ameomba kuweza kuongezewa nguvu ya askari katika wilaya yake ili kuongeza kasi ya kudhibiti kabisa wa wahamiaji haramu, kwani katika Wilaya hiyo kuna maeneo mengi ya vipenyo vya kupitisha wahamiaji haramu kutokana na Jiografia ya wilaya hiyo kwa asilimia kubwa kupakana na nchi ya Kenya ambapo Wahamiaji haramu wengi hutumia maeneo hayo kuingia nchini Kinyume cha sheria.

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACI) Tununasya Ng’ondya alieleza kwamba baada ya kuona changamoto kubwa ya uingiaji wa Wahamiaji Haramu Wilayani Mwanga alishirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na Wilaya ya Mwanga ambapo kupitia Mshauri wa Mgambo Mkoa na Wilaya ya Mwanga walianzisha mafunzo ya Mgambo katika kata za mpakani, ambao sasa askari hao  wanajitolea kwa uzalendo katika kuongeza nguvu ya ulinzi wa mipaka ya nchi yetu kwa utii, uhodari na weledi wa hali ya juu huku wakishirikiana kwa karibu sana na Maofisa na Askari wa Uhamiaji Wilayani hapo.

Akitoa taarifa fupi ya Utendaji kazi ya Wilaya ya Mwanga Afisa Uhamiaji (W) Mrakibu Lydia Moshi alisema Wanashirikiana vyema na kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya pamoja na wananchi kwa ujumla katika mapambano dhidi ya Wahamiaji Haramu, ikiwemo utoaji wa elimu kwa umma juu ya madhara ya Wahamiaji haramu.

Kutokana na kuwa na uhusiano wa karibu na wadau mbalimbali Ofisi ya Uhamiaji Wilaya na Mkoa walitafuta wadau na kuwapata baadhi yao wakiwemo Shirika la Msalaba Mwekundu (Red Cross) Mkoa wa Kilimanjaro ambao nao wamekuwa msaada mkubwa katika kuchangia kupambana na wahamiaji haramu kwani wamesaidia kutoa vifaa mbalimbali kama vile Mahema (Tents) 02 katika maeneo ya Kitobo na Kivisini kwa maana ya kulinda kipenyo cha majini katika Ziwa Jipe na eneo la Kitoghoto.

Ziara ya CGI Dkt. Anna Makakala ni mwendelezo wa ziara zake za kikazi na  baada ya kumaliza Wilayani Mwanga, aliendelea tena Mkoani Kilimanjaro na kukagua maeneo ya mipaka iliyopo Wilaya ya Rombo ikiwemo Tarakea, Holili na Rongai na baadae kuongea na Maafisa na Askari wa Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro.

HABARI PICHA NA MATUKIO
 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akisalimiana na Mkuu wa Wilaya Mwanga Mhe. Thomas Cornel Apson alipowasili Wilayani Hapo kwa ziara ya Kikazi


Mkuu wa Wilaya Mwanga Mhe. Thomas Cornel Apson (kulia) akiwa na Afisa Uhamiaji Wilaya ya Mwanga Mrakibu Lydia Moshi wakati wa Kikao na  Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala (Hayupo Pichani)
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala (Kushoto) akiongea na Mwenyekiti wa Kijiji cha Kitoghoto Bw. Ayubu Ramadhan katika  Kata ya Kivisini Tarafa ya Jepende Wilayani Mwanga kuhusu namna jamii yake inavyoshiriki kupambana na Wahamiaji haramu katika maeneo hayo.




Mwenyekiti wa Kijiji cha Kitoghoto Bw. Ayubu Ramadhan akionesha Hema (Halupo Pichani) walilopokea kutoka katika Shirika la Msalaba Mwekundu Mkoa wa Kilimanjaro

Hema lilitolewa na Shikika la Msalaba Mwekundu Mkoa wa Kilimanjaro ili kusaidia Maafisa, Askari wa Uhamiaji na wale wa Jeshi la Akiba katika kupambana na wahamiaji haramu katika maeneo ya Kitoghoto Wilayani Mwanga


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala  akipokea maelezo ya Moja ya Beacon Ndogo inayotenganisha mpaka wa nchi ya Kenya na Tanzania uliopo Wilayani Mwanga


Moja ya Sehemu ambayo wahamiaji haramu walikuwa wanatumia kuingia nchini kinyume na Sheria sasa Imedhibitiwa












Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akiangalia baadhi ya Mitumbwi iliyokuwa ikitumika kuvushia wahamiaji Haramu katika kijiji cha Mkisha kilichopo kata ya Jipe Wilayani Mwanga






Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akiongea na Wanchi wa Kijiji cha Mkisha kilichopo Kata ya Jipe Wilayani Mwanga




Mmoja wa Wazee Maarufu wa Kijiji cha Mkisha akieleza Changamoto wanazozipata katika eneo hilo


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania CGI Dkt. Anna Makakala akiwasihi wananchi kuendelea kushirikiana na serikali ili kukomesha kabisa wimbi la wahamiaji haramu hapa nchini



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni