Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

28 Januari 2020

UHAMIAJI Mtwara Yamshukuru CGI Kwa Kuongezewa Askari Wapya 20

Mtwara, Tanzania
Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mtwara imetoa shukrani zake za dhati kwa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala kwa kuongezewa nguvu ya askari wapya 20.

Jumla ya askari wapya 20 waliripoti Mkoani Mtwara mwishoni mwa mwezi Disemba mwaka jana 2019 Mara baada ya kumaliza mafunzo ya Uhamiaji katika Chuo cha Uongozi cha Jeshi la Kujenga Taifa JKT-Kimbiji Kilichopo Wilaya ya Kigamboni Jijijini Dar es salaam.

Akitoa Taarifa ya utendaji kazi ya Mkoa, wakati wa ziara ya Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Maurice Kitinusa, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji James Mwanjotile alisema mara baada ya kupata mgao huo aligawa askari hao kwa kila wilaya na vituo vyote vya uhamiaji mkoani hapo kulingana na mahitaji ya sehemu husika.

“Ujio huu wa askari wapya afande umesaidia sana kuongeza ufanisi mkubwa katika utendaji wa shughuli mbalimbali ndani ya Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mtwara, na kwa muda mfupi tu tunaona matunda yake ambapo vitendo vingi vya uhalifu wa Kiuhamiaji vinadhibitiwa ipasavyo, alisema Mwanjotile.

Sanjari na hilo amevishukuru vyombo vingine vya ulinzi na usalama kwa ushirikiano wanaoutoa katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya kiuhamiaji ndani ya mkoa wa mtwara  bila kuwasahau wananchi wa mkoa huo ambao wamekuwa msaada mkubwa wa kutoa taarifa za wahamiaji haramu na kusaidia kudhibiti vitendo hivyo.

Ikumbukwe kuwa mafanikio yote hayo yanatokana na Juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano chini ya  Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli ambae ndie aliyetoa kibali cha Kuajiri Jumla ya Askari wapya 400 waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT, Oparesheni Kikwete na Oparesheni Magufuli Kujitolea na baadae kujiunga na Mafunzo ya Idara ya Uhamiaji, tayari askari hao wametawanywa nchi nzima Tanzania bara na Zanzibar tayari kwa kulitumikia Taifa lao kwa utii, uzalendo weledi na uhodari.


  HABARI PICHA NA MATUKIO
Kamishna wa Uhamiaji aneyesimamia Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Maurice Kitinusa akisalimiana na Maofisa askari na Watumishi wa Umma Mkoani Mtwara wakati wa ziara yake hivi karibuni
Kamishna wa Uhamiaji aneyesimamia Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Maurice Kitinusa akisalimiana na Maofisa askari na Watumishi wa Umma Mkoani Mtwara wakati wa ziara yake hivi karibuni



Kamishna wa Uhamiaji aneyesimamia Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Maurice Kitinusa akisaini kitabu cha wageni Mkoani Mtwara wakati wa ziara yake hivi karibuni.
Picha na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Mtwara
Askari wapya wa Idara ya Uhamiaji Tanzania
Askari wapya wa Idara ya Uhamiaji Tanzania
Picha na Maktaba Kutoka Kitengo cha Uhusiano Makao Makuu yan Uhamiaji

Maoni 1 :