Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

22 Januari 2020

Uhamiaji Iringa yakamata tena Wahamiaji Haramu


Iringa, Tanzania
Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Iringa inawashikilia Watuhumiwa  (09) kwa makosa ya kiuhamiaji ambapo (07) ni  raia wa Ethiopia, (01) raia wa Kenya mwenye asili ya Somalia na  (01) raia wa Tanzania ambae ni dereva.

Akizungumza na Waandishi wa habari mapema wiki hii, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa - Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji, Agnes Michael Luziga  alisema, watuhumiwa  hao wamekamatwa  eneo la Mtera getini na Askari wa Uhamiaji waliokuwa kwenye doria ya kawaida.  

Watuhumiwa hawa wamekamatwa kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha Sheria ya Uhamiaji Sura ya 54 (Immigration Act Cap 54 RE 2016) pamoja na kanuni zake na watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani baada ya upelelezi wa tuhuma zao kukamilika, aliongeza Kamishna Msaidizi Mwandamizi Luziga.

Baada ya kuhojiwa na kukaguliwa ilibainika kuwa watuhumiwa hao walikuwa na  pasipoti za kughushi  za Kenya na Ethiopia zikiwa na  vibali vya kughushi na wameingia nchini kupitia njia za panya wakitokea nchini Kenya wakipita kuelekea  nchini Afrika Kusini.

Watuhumiwa hao walitumia gari binafsi aina ya Noah lenye namba za usajili T656 DNP lililokuwa likiendeshwa na dereva raia wa Tanzania Mosses Apendavyo Mbwambo, Watuhumiwa wengine ni Isse Aliye Abdi, Hussein Hirsi Ali, Hassan Maalim Adan, Jama Abdulmalik Yuune, Hussein Siyad Ali,  Mohhamed Hassan Tikki, Ali Muktar Abdulkadir na Osman Mohamed Ali.

Aidha, Idara ya Uhamiaji inatoa  wito  kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri pamoja na madereva kuaacha mara moja tabia na  tamaa za kujishughulisha na  biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu kwani ni kinyume na sheria za nchi na hatari kwa usalama wa nchi yetu.

HABARI PICHA NA MATUKIO

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji Agnes Michael Luziga Afisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa  


Watuhumiwa wa Makosa ya Kiuhamiaji waliokamatwa Iringa



Gari aina ya Noah lililotumika kusafirishia wahamiaji Haramu


Wahamiaji haramu wakifikishwa katika kituo cha polisi Iringa
(Picha zote na Ofisi ya Uhusiano - Uhamiaji Iringa)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni