Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

06 Januari 2020

Uandikishaji Vitambulisho vya Taifa: Uhamiaji Arusha yaweka Kambi Uwanja wa Sheikh Amri Abeid

 Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa wameanzisha Oparesheni maalumu ili kuwezesha wananchi wengi kupata Vitambulisho vya Taifa kwa wakati kwa kuweka kambi katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Arusha Naibu Kamishna wa Uhamiaji Abdallah Towo anaongoza timu ya maafisa na askari wa Uhamiaji katika kutekeleza oparesheni hiyo. Katika oparesheni hii, Idara ya Uhamiaji ina jukumu la kuthibitisha uraia wa mwombaji wa kitambulisho cha Taifa kabla hajasajiliwa na kupewa namba na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Vitambulisho hivyo pamoja na kuwa utambulisho kwa raia wa Tanzania na wageni wakazi, pia vinatumika katika usajili wa laini za simu ambapo awali usajili ulikuwa ufike kikomo tarehe 31 Disemba 2019 lakini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliongeza siku 20 kuanzia Januari Mosi hadi 20, 2020.



Afisa Uhamiaji Mkoa Arusha DCI Abdallah Towo akisajili jina la mmoja wa waombaji wa vitambulisho kwenye rejista maalumu wakati wa zoezi la uandikishaji wananchi jijini Arusha linaloendelea katika uwanja wa Sheikh AMri Abeid.

Huduma zikiendelea katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha ambapo mamia ya wakazi wa jiji hilo wameitikia wito kuja kujiandikisha ili kupata vitambulisho vya Taifa.

Baadhi ya wakazi wa jiji la Arusha waliofika uwanjani kuhudumiwa

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mh. Fabian Daqarro akijadiliana jambo na Afisa Uhamiaji Mkoa Arusha Naibu Kamishna Abdallah Towo katika zoezi la uandikishaji Vitambulisho vya Taifa linaloendelea katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni