Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

27 Januari 2020

Kamishna Kitinusa Apeleka Ujumbe wa CGI Mtwara na Kumshukuru Rais Magufuli kwa Kuajiri Askari wapya 400.


Mtwara, Tanzania
Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Maurice David Kitinusa mapema wikii hii amefanya ziara ya siku mbili katika Mkoa wa Mtwara na wilaya zake huku akibeba ujumbe wa Kamishana Jenarali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala.

Akiongea na Maafisa, Askari na Watumishi wa Idara ya Uhamiaji Mkoani hapo alisema Kamishna Jenerali wa Uhamiaji anamshukuru Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuridhia kuajiri askari wapya 400 waliohitimu mafunzo yao mwezi Disemba mwaka jana 2019  katika Chuo cha Uongozi chaJeshi la Kujenga Taifa-Kimbiji kilichopo wilaya ya Kigamboni Jijini  Dar es salaam, na tayari  walishapangiwa vituo mbalimbali vya kazi nchi nzima na wanachapa kazi ipasavyo.

Mbali na idadi hiyo kuongezeka bado tuna uhitaji mkubwa wa watumishi ndani ya idara yetu kwani malengo ni kufikia askari elfu ishirini (20,000).

Hivyo kutokana na upungufu huo kamishina Jenerali amewataka watumishi wote waliopo kufanya kazi kwa bidii, weledi, uzalendo utii na uhodari wa hali ya juu wakati changamoto hiyo ikiendelea kutatuliwa kama ilivyooneshwa nia na Rais Magufuli.

Aidha ameendelea kusisitiza Utoaji wa huduma bora na ukusanyaji wa maduhuli ya serikali na kuhakikisha Idara inatimiza malengo yake ya kukusanya maduhuli kwa ajili ya maendeleo na uchumi wa Taifa.
Katika ujumbe huo kamishna Jenerali wa Uhamiaji amewaasa Maafisa, Askari, na Watumishi wote ndani ya Idara ya Uhamiaji kujiepusha na rushwa na kufanya kazi kwa weledi zaidi.

Kutokana na tatizo la wahamiaji haramu ndani ya nchi, Kamishina Jenerali amewataka askari na watumishi wengine wa Idara ya Uhamiaji kuhakikisha wanakabiliana na tatizo hilo kwa kuendesha Oparesheni maalumu, akifafanua ujumbe huo Kamishna Maurice Kitunusa ametoa agizo la kufanyika kwa Oparesheni maalumu ya kuwabaini wahamiaji haramu waliopo ndani ya nchi na kuwachukulia hatua ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani.

Pia amesisitiza kutumia vyombo vya habari nchini yaani T.V, redio, magazeti na mitandao ya kijamii ili kuuhabarisha umma juu ya kinachoendelea katika oparesheni hiyo na Kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya madhara ya kuruhusu wahamiaji haramu katika nchi yetu ambapo ni hatari kwa usalama wa Taifa na Dunia kwa ujumla.

Kamishna Kitunusa aliwasili Mkoani Mtwara akitokea Mkoa wa Lindi na Kupokelewa na Mwenyeji wake Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi James A. Mwanjotile huku akikagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo Jipya la Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mtwara na baadae kutembelea daraja la umoja linalotenganisha Wilaya ya Nanyumbu na Nchi ya Msumbiji.


HABARI PICHA NA MATUKIO
Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Maurice David Kitinusa akiwasilikatika Ofisi za Uhamiaji Mkoani Mtwara
Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Maurice David Kitinusa (katikati) akiwa katika ofisi ya Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara tayari kwa kupokea taarifa ya Uhamiaji Mkoa kutoka kwa Mwenyeji wake Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi James A. Mwanjotile 

Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Maurice David Kitinusa akisalimiana na Maofisa na Askari wa Ofisi ya Uhamiji Wilaya ya Masasi

Pichani Ujenzi wa Jengo Jipya la Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mtwara ukiendelea.



Kamishna Kitinusa alipotembelea daraja la umoja linalotenganisha Wilaya ya Nanyumbu na Nchi ya Msumbiji.
Daraja la umoja linalotenganisha Nchi ya Tanzania na Msumbiji katika  Wilaya ya  Nanyumbu.



Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Mkoa wa Mtwara
Baadhi ya Askari wa Uhamiaji Wakimsikiliza kwa makini Kamishana Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala (Hayupo Pichani) alipowatembelea na kukagua maendeleo yao siku chache kabla ya sherehe ya kumaliza mafunzo yao ya Uhamiaji katika Chuo cha Uongozi wa Kijeshi JKT- Kimbiji.

Maoni 1 :