Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

30 Januari 2020

UHAMIAJI Iringa Kinara wa Kukamata Wahamiaji Haramu


Iringa, Tanzania

Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Iringa kwa mara nyingine imekamata wahamiaji haramu (07) raia wa Ethiopia mapema leo hii asubuhi baada ya kutelekezwa na kiongozi wao.

Akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji (SACI) Agnes Michael Luziga alisema, watuhumiwa wote wamekamatwa eneo la Igumbilo lililopo karibia na Kituo Kikuu cha mabasi Iringa na Kikosi Maalumu cha doria cha Askari wa Uhamiaji wakati wakitekeleza majukumu yao ya kila siku.

Baada ya kuhojiwa imebainika kuwa watuhumiwa hao walikuwa wametelekezwa na wenyeji wao na walikuwa wanapita katika njia za panya maeneo ya nje kidogo ya Manispaa ya Iringa na walikuwa wanaelekea nchini Afrika ya Kusini kupitia Malawi, aliongeza Kamishna Msaidizi Mwandamizi Luziga.

Watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha Sheria ya Uhamiaji Sura 54, Rejeo la Mwaka 2016 pamoja na Kanuni zake.

Aidha, Idara ya Uhamiaji inatoa wito kwa watu wasiowadilifu na wanaojihushisha na biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu kuacha mara moja.

Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Iringa inaendelea kufanya doria na oparesheni mbalimbali kwa lengo la kuwabaini na kuwakamata watuhumiwa wote wanaoishi nchini kinyume cha Sheria na kuwafikisha Mahakamani na hatimaye kuwaondosha nchini.

Ikumbukwe kuwa ndani ya mwezi mmoja tu wa Januari 2020 Uhamiaji Mkoa wa Iringa imefanikiwa kukamata wahamiaji haramu zaidi ya mara tatu mfululizo.
HABARI PICHA NA MATUKIO
Afisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji (SACI) Agnes Michael Luziga
Afisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji (SACI) Agnes Michael Luziga (Kulia) akiwa na Afisa Uhamiaji Msaidizi Mkoa Kamishna Msaidizi (ACI) Peter Joseph Kimario 
Watuhumiwa waliokamatwa








(Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Mkoa wa Iringa)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni