Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

09 Machi 2020

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara Afanya Ziara na Kugawa Vitendea kazi

Mtwara, Tanzania
Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi James Mwanjotile amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya zote za Mkoa wa Mtwara yaani Masasi, Newala, Nanyumbu na Tandahimba.

Lengo kuu la ziara hiyo ni kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kiutendaji katika wilaya hizo na Mkoa kwa ujumla. 

Akizungumza na Maafisa, Askari na watumishi raia wa Uhamiaji katika Wilaya hizo, Kamishna Msaidizi Mwanjotile, amesisitiza kuhakikisha kuwa wanatunza vifaa vyote vya Ofisi pamoja na  kufanya kazi kwa weledi wakizingatia Sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali.

Aidha, amewakumbusha Maafisa Uhamiaji Wilaya kuendelea kutoa elimu kwa umma ambapo, Mkoa wa Mtwara tayari umeshaanza kuandaa programu maalum za Elimu ya Uhamiaji na Uraia kwa Umma kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi hususani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, na kuhakikisha wanashughulikia changamoto za uraia zitakazo jitokeza wakati wa kipindi cha uchaguzi, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala alilolitoa hivi karibuni Jijini Dodoma.

Vilevile Kamishna Msaidizi Mwanjotile ametoa wito kwa Maafisa Uhamiaji Wilaya wote wa Mkoa huo kuhakikisha kuwa wageni wote wanaoishi katika maeneo yao wanafuata sheria, sanjari na kusisitiza kuongeza udhibiti wa uingiaji na utokaji wa wageni na raia wa Tanzania katika mipaka yote ya Mkoa huo kwa kuimairisha doria na misako ya wahamiaji haramu kote nchini ili kuhakikisha kuwa nchi inabaki salama na wahamiaji haramu hawanufaiki na rasilimali zetu.

HABARI PICHA NA MATUKIO 
Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi James Mwanjotile akiwa katika moja ya Ofisi ya Uhamiaji Wilaya wakati wa ziara yake.




Baadhi ya vitendea kazi vikishushwa katika moja ya Wilaya za Mkoa wa Mtwara  (Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Mkoa wa Mtwara)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni