Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

16 Machi 2020

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YATEMBELEA UJENZI WA JENGO LA UHAMIAJI MAKAO MAKUU

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Victor Mwambalaswa imetembelea na kukagua maendeleo ya Ujenzi wa  jengo la Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji jijini Dodoma leo Jumatatu Machi 16, 2020.

Kamati hiyo ambayo ilipokelewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. George Simbachawene , Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala, Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Johari  Masoud Sururu, Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha) Edward Chogero pamoja na Maafisa Uhamiaji Waandamizi katika eneo la ujenzi wa mradi huo.

Mhandisi Kanali Zabron Mahenge ambaye ni Meneja Mradi kutoka Jeshi la Kujenga Taifa aliieleza Kamati hiyo kuwa ujenzi unaendelea vizuri pamoja na kuwepo changamoto ndogo ndogo na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.

Akitoa taarifa ya maendeleo ya Ujenzi huo, Mhandisi wa Mradi David Pallangyo alisema hadi sasa ujenzi umefikia hatua nzuri ambapo sakafu ya ghorofa ya tatu imekamilika kwa 60% na ujenzi utakamilika kwa muda uliopangwa.

Mwenyekiti wa Kamati  ya Bunge  Mhe.Mwambalaswa alimpongeza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,  Kamishna Jenerali pamoja na wahandisi  kwa usimamizi mzuri ujenzi wa Jengo hilo na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili ujenzi ukamilike kama ilivyopangwa.

Nae Mjumbe wa Kamati hiyo ya Bunge Mhe. Almas Maige  hakusita kutoa pongezi kwa  Wizara ya mambo ya Ndani na Idara ya Uhamiaji kwa ujenzi wa jengo hilo la Makao Makuu ambalo ni kubwa na la kisasa pindi litakapokamilika.

Ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji jijini Dodoma lenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 20 unaojengwa na  Suma JKT unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.

Ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya  Idara ya Uhamiaji jijini Dodoma ukiendelea

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akimlaki Katibu Mkuu Mambo ya Ndani Mh. Christopher Kadio alipowasili katika eneo la ujenzi wa Makao Makuu ya uhamiaji jijini Dodoma leo tarehe 16 Machi 2020.

Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Johari Sururu akiongea na Katibu Mkuu mambo ya Ndani ya Nchi

Katika kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya Corona, Katibu Mkuu akinawa mikono kwenye eneo la ujenzi

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akinawa mikono yake ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona katika eneo la ujenzi wa ofisi za Uhamiaji Makao Makuu jijini Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. George Simbachawene akilakiwa na Makamishna wa Uhamiaji wakiongozwa na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji 

Waziri Simabachawene akinawa mikono yake kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona




Waziri Simbachawene akiongea na Wahandisi na mafundi wanaojenga jengo la Uhamiaji Makao Makuu Dodoma


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Mhe. Mwambalaswa akishuka katika basi lililowabeba wajumbe wa Kamati hiyo walipowasili katika eneo la Ujenzi 

Wanakamati wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakinawa mikono yao 


Mh. Vuai Nahodha akinawa mikono yake kujikinga na Corona wakati walipowasili eneo la Ujenzi wa Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dodoma

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge akioneshwa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la Uhamiaji Makao Makuu na Waziri Simbachawene

Mwenyekiti wa Kamati na Wajumbe wakisoma taarifa ya Maendeleo  ya Ujenzi wa Makao Makuu ya Uhamiaji




Mjumbe wa Kamati Mhe. Almas Maige akichangia jambo wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dodoma

Mwenyekiti wa Kamati akitoa neno alke wakati wa ziara ya kamati yake


Ukaguzi wa ujenzi ukiongozwa na Wahandisi David Pallangyo na Kanali Mahenge



Wajumbe wakikagua sakafu ya chini ya jengo (Basement) katika jengo la Uhamiaji Makao Makuu





Wajumbe wa kamati wakikagua ujenzi wa sakafu ya ghorofa ya tatu unaondelea

Mh. Almas Maige akikagua hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa sakafu ya ghorofa ya tatu





Sehemu ya Wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge wakishuka ngazi za Jengo la Uhamiaji Makao Makuu linaloendelea kujengwa jijini Dodoma



Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Ndani mara baada ya Kamati ya Kudumu ya Bunge kumaliza ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dodoma



Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Johari Sululu na Kamishna wa Uhamiaji Edward Chogero (Utawala na Fedha) ni miongoni mwa waliohudhuria ukaguzi huo



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni