Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

13 Machi 2020

CGI Dkt. Anna Makakala Akutana na Ubalozi wa Japani nchini Tanzania


Dar es salaam, Tanzania 
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala mapema leo hii katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam amepokea ugeni kutoka Ubalozi wa Japani nchini Tanzania na kufanya mazungumzo.


Ugeni huo umekuja na ujumbe wa kuwasilisha hati mpya za kusafiria (Japanese Travel Documents Model 2020) zilizoboreshwa ambazo zinatumika hivi sasa nchini Japani ikiwa na lengo la kusambaza toleo lao jipya la Pasipoti kwa nchi mbalimbali duniani  ili ziweze kutambulika pale raia wao wanapoingia nchini, na huu ni utaratibu wa kawaida kabisa kwa kila nchi inapozindua pasipoti yake mpya basi lazima ipekeleka mfano wa hati hizo mpya (Travel Documents Model) katika Mataifa mbalimbali ili ziweze kujulikana na kutumika Kimataifa.

Dkt. Makakala ameishukuru serikali ya Japani kwa kuendeleza Mahusiano mazuri yaliyopo hususani katika masuala ya kiuhamiaji na kusaidiana katika kutatua changamoto mbalimbali za kiuhamiaji zinazoweza kujitokeza kwa watanzania na raia wa Japani ikiwa sanjari na utekelezaji wa mfumo wa  Uhamiaji Mtandao.

Mfumo wa Uhamiaji Mtandao ni Mfumo unaounganisha mifumo yote ya utoaji huduma kwa njia za kielektroniki, hivyo kupitia Uhamiaji Mtandao huduma mbalimbali za kiuhamiaji kama vile Pasipoti, Vibali, Visa, pamoja na usimamizi na udhibiti wa mipaka kielekroniki hutolewa.

HABARI PICHA NA MATUKIO

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala (Kulia) akipokea baadi ya nyaraka za Pasipoti mpya ya Japani (Japanese Travel Documents Model 2020) kutoka kwa mwakilishi wa Ubalozi wa Japani.
Muonekano wa Hati mpya za kusafiria (Japanese Travel Documents Model 2020) zilizoboreshwa ambazo zinatumika hivi sasa nchini Japani


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala (Kulia) akimsikiliza Mwakilishi wa Ubalozi wa Japani Nchi Tanzania akitoa Maelezo ya Pasipoti mpya ya Japani




Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala (Kulia) akioneshwa baadhi ya nyaraka zinazothibitisha ubora wa viwango vya Kimataifa katika Pasipoti mpya ya Japani 


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala (Kulia) akimkabidhi Jarida la Uhamiaji Mwakilishi wa Ubalozi wa Japani Nchini Tanzania.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala (Kulia) akibadilishana Mawasiliano na wawakilishi wa Ubalozi wa Japani baada ya kumaliza maungumzo.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Peter Makakala (Kulia) akiagana na Ugeni kutoka Ubalozi wa Japani nchini Tanzania, Pasipo kushikana mikono ikiwa ni utekelezaji wa kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa  hatari wa Korona (Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni