Jeshi la Uhamiaji
Tanzania kwa kushirikiana na Ubalozi wa Canada imeendesha Mafunzo ya Kuwajengea
uwezo Maafisa na askari wa Kituo cha Uhamiaji Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius
Nyerere (JNIA)
Mafunzo hayo ya siku tatu yanahusisha jumla ya Maafisa na Askari 31 ambapo yanafanyika katika Ofisi ndogo za makao makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar e
salaam, na yanatarajiwa kumalizika kesho tarehe 13 Machi 2020.
Mafunzo hayo yana lengo
kuu la kuwajengea uwezo mafisa na askari katika kutekeleza majukumu yao ya
kuhudumia wageni na raia wa Tanzania katika vituo mbalimbali vya kuingia na
kutoka nchini sanjari na kudhibiti
uingiaji wa Wahamiaji haramu.
Mafunzo hayo
yameongozwa na Bwana David Henry kutoka ubalozi wa Canada nchini Tanzania
ambapo Makao yake Makuu yapo Nairobi nchini Kenya.
Bwana Henry amefundisha
mambo mbalimbali yanayohusu ukaguzi wa nyaraka mbalimbali za kiuhamiaji kwa
kutumia njia mbalimbali za kisasa ili kuwabaini wahalifu wanaoweza kughushi
nyaraka kama vile Pasipoti, Visa na Vibali vya ukaazi, sanjari na kufanya
mahojiano kwa kina na mgeni au raia wa Tanzania kwa njia za kisasa zaidi wanapokuwa
katika mipaka (Entry Points).
Mafunzo ya aina hii
hutolewa mara kwa mara kwa maafisa na askari wa Uhamiaji Tanzania, chini ya
kitengo cha mafunzo.
Aidha Mafunzo ya aina
hii husaidia Maafisa na Askari kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia,
hasa katika kipindi hiki cha utekelezaji wa Uhamiaji Mtandao ambapo unaakisi
mabadiliko ya kiteknolojia duniani ambayo yanakwenda kwa kasi na kutumia
kiwango cha juu cha TEHAMA katika huduma mbalimbali na hatimae kuendana na utoaji
wa huduma za kiuhamiaji zenye viwango vya kimataifa na kuimarisha ulinzi na
usalama wa nchi na mipaka yake.
HABARI PICHA NA MATUKIO
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Uhamiaji kutoka Kituo cha (JNIA) Wakipatiwa mafunzo maalumu ya kujengewa uwezo |
Bwana David Henry Mkufunzi kutoka Ubalozi wa Canada Nchini Tanzania akifundisha |
Baadhi ya Maafisa Uhamiaji wakifuatilia kwa makini mafunzo yanayotolewa na Bwana David Henry Kutoka Ubalozi wa Canada |
Baadhi ya Maafisa Uhamiaji wakiangalia kwa makini moja ya kifaa cha kuchunguzia Pasipoti ili kutambua uhalali wake |
Mafunzo yakiendelea kutolewa |
Mratibu wa Mafunzo Uhamiaji Mkaguzi Nabwike Joseph (Kushoto) akiagana na Mkufunzi Bwana David Henry Kutoka Ubalozi wa Canada (Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu). |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni