Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

12 Machi 2020

Zaidi ya Maafisa na Askari 30 wa Jeshi la Uhamiaji Tanzania kutoka (JNIA) Wapatiwa Mafunzo Kabambe

Dar es salaam, Tanzania
Jeshi la Uhamiaji Tanzania kwa kushirikiana na Ubalozi wa Canada imeendesha Mafunzo ya Kuwajengea uwezo Maafisa na askari wa Kituo cha Uhamiaji  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA)

Mafunzo hayo ya siku tatu yanahusisha jumla ya Maafisa na Askari 31 ambapo yanafanyika katika Ofisi ndogo za makao makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar e salaam, na yanatarajiwa kumalizika kesho tarehe 13 Machi 2020.

Mafunzo hayo yana lengo kuu la kuwajengea uwezo mafisa na askari katika kutekeleza majukumu yao ya kuhudumia wageni na raia wa Tanzania katika vituo mbalimbali vya kuingia na kutoka nchini  sanjari na kudhibiti uingiaji wa Wahamiaji haramu.

Mafunzo hayo yameongozwa na Bwana David Henry kutoka ubalozi wa Canada nchini Tanzania ambapo Makao yake Makuu yapo Nairobi nchini Kenya.

Bwana Henry amefundisha mambo mbalimbali yanayohusu ukaguzi wa nyaraka mbalimbali za kiuhamiaji kwa kutumia njia mbalimbali za kisasa ili kuwabaini wahalifu wanaoweza kughushi nyaraka kama vile Pasipoti, Visa na Vibali vya ukaazi, sanjari na kufanya mahojiano kwa kina na mgeni au raia wa Tanzania kwa njia za kisasa zaidi wanapokuwa katika mipaka (Entry Points).

Mafunzo ya aina hii hutolewa mara kwa mara kwa maafisa na askari wa Uhamiaji Tanzania, chini ya kitengo cha mafunzo.

Aidha Mafunzo ya aina hii husaidia Maafisa na Askari kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia, hasa katika kipindi hiki cha utekelezaji wa Uhamiaji Mtandao ambapo unaakisi mabadiliko ya kiteknolojia duniani ambayo yanakwenda kwa kasi na kutumia kiwango cha juu cha TEHAMA katika huduma mbalimbali na hatimae kuendana na utoaji wa huduma za kiuhamiaji zenye viwango vya kimataifa na kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi na mipaka yake.  

HABARI PICHA NA MATUKIO
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Uhamiaji kutoka Kituo cha (JNIA) Wakipatiwa mafunzo maalumu ya kujengewa uwezo

Bwana David Henry Mkufunzi kutoka Ubalozi wa Canada Nchini Tanzania akifundisha 

Baadhi ya Maafisa Uhamiaji wakifuatilia kwa makini mafunzo yanayotolewa na Bwana David Henry Kutoka Ubalozi wa Canada



Baadhi ya Maafisa Uhamiaji wakiangalia kwa makini moja ya kifaa cha kuchunguzia Pasipoti ili kutambua uhalali wake


Mafunzo yakiendelea kutolewa 

Picha ya Pamoja, Katikati ni Mkufunzi kutoka Ubalozi wa Canada Bwana David Henry na Kushoto kwake  ni Mratibu wa Mafunzo Mkaguzi wa Uhamiaji Nabwike Joseph wakiwa na Maafisa na Askari Waliopatiwa Mafunzo hivi karibuni

Mratibu wa Mafunzo Uhamiaji Mkaguzi Nabwike Joseph (Kushoto) akiagana na Mkufunzi Bwana David Henry Kutoka Ubalozi wa Canada (Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni