Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

04 Machi 2020

Dkt. Makakala awataka Maafisa Uhamiaji Mikoa Yote Nchini Kutoa Elimu ya Uhamiaji na Uraia kwa Wananchi


 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dtk. Anna Peter Makakala amewataka Maafisa Uhamiaji Mikoa wote nchini kujita zaidi katika kutoa Elimu ya Uhamiaji na Uraia kwa Watanzania. Hayo ameyasema leo Jumatano tarehe 4 Machi 2020 alipotembelea Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Dodoma kwa ziara ya Kikazi.



Akizungumza na Maafisa na Askari wa Uhamiaji, Dkt. Makakala amewata Maafisa Uhamiaji Mikoa wote nchini kuandaa programu maalum za Elimu ya Uraia kwa Umma kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi hususan katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.


"Nchi yetu Mwaka huu inafanya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani hivyo ni rai yangu kwa Maafisa Uhamiaji Mikoa kushirikiana vyema na Tume ya Uchaguzi kwa kutoa elimu ya uraia kwa wananchi na kushughulikia changamoto za uraia zitakazo jitokeza wakati wa kipindi cha uchaguzi na kuhakikisha kuwa wanazipatia majibu kwa  wakati" amesema Dkt. Makakala.


Vilevile Dkt.  Makakala ametoa wito kwa Maafisa Uhamiaji Mikoa hao  kuhakikisha kuwa Wageni wote wanaoishi katika maeneo yao wanaishi kwa kufuata sheria.


Aidha, Maafisa Uhamiaji wote wametakiwa kuimairisha Doria na Misako ya Wahamiaji haramu kote nchini ili kuhakikisha kuwa nchi yetu inabakia kuwa salama na Wahamiaji haramu hawanufaiki na rasilimali zetu.


Kwa Upande wake Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Divisheni ya Vibali vya Ukaazi, Visa na Pasi, Mary Palmer (ndc) amewataka raia wa kigeni wote wanaoishi nchini kuhakikisha kuwa wana vibali vya Ukaazi.


Kamishna Palmer amesisitiza kuwa wageni wanaohitaji kuingia na kuishi nchini kwa madhumuni mbalimbali wanaweza kufanya maombi, kulipia na kupokea nakala za vibali vyao kwa njia ya mtandao.


Awali akitoa taarifa ya Utendaji kazi ya Mkoa, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Abdallah Katimba ameeleza kuwa Mkoa wa Dodoma umeimarisha Doria na Misako dhidi ya Wahamiaji haramu, na pia Mkoa umejipanga vyema kutoa Elimu ya Uraia kwa Watanzania.



Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akiongea na mmoja wa wateja wa huduma za Uhamiaji katika ofisi ya uhamiaji mkoa Dodoma.










Baadhi ya Askari na Maafisa wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji alipofanya ziara katika Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Dodoma.

Afisa Utumishi Mkuu Ndugu Mulegi Majogoro akiongeaa wakati wa kikao cha Watumishi wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Dodoma na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji alipozuru ofisi ya Mkoa jijini Dodoma leo tarehe 04 Machi 2020.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni