Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

06 Machi 2020

UHAMIAJI Iringa Yatekeleza Agizo la Kamishina Jenerali wa Uhamiaji


Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Iringa imetekeleza agizo la Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala alilolitoa mapema wiki hii akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Dodoma kwa Maafisa Uhamiaji Mikoa yote nchini kutoa elimu ya Uhamiaji na Uraia kwa watanzania kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020.

Akizungumzia kuhusu Utekelezaji huo, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Agness Luziga amesema Maafisa na Askari wa Uhamiaji Mkoa wa Iringa wanatembelea Maeneo mbalimbali Mkoani humo kwa ushirikiano na vyombo vya habari vikiwemo Vituo vya Radio, Televisheni na Mitandao ya Kijamii kutoa elimu ya Uhamiaji na Uraia hasa kuelekea kipindi hiki muhimu cha Uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani.

Kwa kushirikiana na Kituo cha Redio Furaha Fm 96.7 kilichopo katika Manispaa ya Iringa, wametoa elimu ya Uraia kwa Wananchi wa Mkoa wa Iringa na Tanzania kwa ujumla.

Kupitia Kipindi hicho Wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali na kupatiwa ufafanuzi kuhusu huduma za Uhamiaji na Uraia.

Afisa Uhamiaji Mkoa huyo amesisitiza kuwa zoezi hilo ni endelevu na litashirikisha Viongozi wa Serikali za Mitaa, Tume ya Uchaguzi pamoja na Jamii kwa ujumla.


HABARI PICHA NA MATUKIO

Maafisa Uhamiaji Mkoa wa Iringa wakiwa ndani ya Kituo cha Redio Furaha Fm Kutekeleza Agizo la CGI la kutoa elimu kwa Umma kuhusu Huduma za Uhamiaji na Uraia katika Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2020
(Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Mkoa wa Iringa)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni