Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

10 Machi 2020

UHAMIAJI Tanzania Yatoa Mafunzo Kwa Mabalozi Wateule

Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Divisheni ya Vibali vya Ukaazi, Pasi na Visa, Mary Palmer (ndc) ameongoza Ujumbe wa Mabalozi 03 katika Mafunzo ya huduma mbalimbali za kiuhamiaji zinazotolewa katika Balozi za Tanzania Nje ya Nchi.

Waheshimiwa Mabalozi waliohudhuria mafunzo hayo ni Maj. Gen. Jacob Kingu, Kamishna Jenerali (Mstaafu) wa Magereza  Phaustine Kasike na Dkt. John Simbachawene ambao wameteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Katika mafunzo hayo, mada mbalimbali ziliweza kuwasilishwa na Maafisa kutoka Idara ya Uhamiaji hususani Pasipoti, Visa za kielektroniki, pamoja na Mifumo inayotumika katika utoaji wa Pasipoti na Visa za kieletroniki.

Aidha, Waheshimiwa Mabalozi walipata fursa ya kuuliza maswali na kujibiwa ipasavyo na watoa mada sanjari na kufurahishwa na namna mifumo mbalimbali ya Uhamiaji inavyofanya kazi  na kurahisisha utoaji wa huduma za uhamiaji kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa.

Kwa upande wake Balozi Mteule wa Tanzania Meja Jenerali Jacob Kingu kwa niaba ya mabalozi wenzake alimshukuru na Kumpongeza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji kwa mafunzo waliyoyapata.

Pia ameongeza kuwa, mafunzo hayo yamewajengea uwezo wa kwenda kufanya kazi kwa ufanisi hususani katika kuwahudumia Watanzania waishio nje ya nchi na wageni wanaoingia hapa nchini kwa madhumuni mbalimbali ikiwemo utalii, matembezi, Biashara na uwekezaji.

Mafunzo hayo Yamefanyika katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya  Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam na ni muendelezo wa Elimu ya Uhamiaji na Uraia inayotolewa na Idara ya Uhamiaji kwa Makundi mbalimbali ikiwemo Wanadiplomasia.

 HABARI PICHA NA MATUKIO
Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Divisheni ya Vibali vya Ukaazi, Pasi na Visa, Mary Palmer (ndc) akitoa utangulizi wa Mafunzo kwa Mabalozi Wateule.


Balozi Mteule Maj. Gen. Jacob Kingu, akisikiliza kwa makini elimu anayopatiwa kutoka kwa Maafisa Uhamiaji



Mkaguzi wa Uhamiaji Gerald Kawishe akifundisha somo la Uraia na Pasipoti kwa Mabalozi wateule

Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji Godbless Swai akifundisha somo la Vibali vya Ukaazi na Visa kwa Mabalozi wateule (hawapo pichani)

Mabalozi wateule wakisoma kwa vitendo namna ya kukagua nyaraka mbalimbali za Kiuhamiaji
Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji  Ritha Muumba akifundisha Huduma za kibalozi (Consular Services) kwa Mabalozi wateule

Afisa TEHAMA Mwandamizi Rodern Mtulo Akisikiliza kwa makini maswali kutoka kwa mabalozi wateule baada ya kupata mafunzo ya Huduma za Kiuhamiaji


Picha ya Pamoja baada ya kumaliza Mafunzo
Mabalozi Wateule wakiagana baada ya kumaliza mafunzo katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji  Kurasini Dar es salaam (Picha na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni