Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

05 Machi 2020

Ziara Ya Katibu Mkuu Mambo Ya Ndani: Uhamiaji Waaswa Kulinda Taswira Nzuri Ya Idara Yao


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ndg. Christopher Kadio amefanya ziara ya Kikazi Ofisi ya Uhamiaji Makao Makuu na kuzungumza na Menejimenti, Maafisa, Askari na Watumishi raia wa Uhamiaji alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Uhamiaji - Dodoma, kwa lengo la kuona na kuzipatia ufumbuzi changamoto zinaikabili Idara ya Uhamiaji na kuomba ushirikiano wa kutatua kwa pamoja.

Akizungumza na Watumishi hao, Katibu Mkuu Kadio amesisitiza utendaji kazi wenye kuzingatia weledi, nidhamu na unyenyekevu hasa wakati wa kupokea mrejesho wa huduma za Uhamiaji hususan kupitia malalamiko ama ukosoaji wa namna yoyote toka kwa watu Wananchi.

"Kupokea malalamiko na kuyafanyia kazi ni njia nzuri ya kutunza taswira ya taasisi na ama kulinda hadhi ya Idara yenu” amesisitiza 

Aidha, Katibu Mkuu amewataka watumishi hao kutoa maoni yao na ushauri kwa lengo kuboresha ufanisi wa Utendaji kazi.

Mtendaji Mkuu huyo wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi amesisitiza kuwa endapo Idara itafanikiwa kuzitatua changamoto zinazioikabili itakuwa ni Mafanikio kwa Wizara na Serikali kwa ujumla.

Pia Katibu Mkuu Kadio ameipongeza Idara kwa kuboresha kwa kiwango kikubwa utoaji wa huduma za Paspoti na kuwaasa kuwa kazi kubwa waliyonayo ni kulinda mafanikio hayo na kuendelea kuboresha zaidi ya ubora uliopo sasa.

Akihitimisha mazungumzo yake Ndugu Kadio ameahidi kukutana na watumishi mbalimbali walio chini ya Wizara na taasisi zake mara nyingi iwezekanavyo kwa lengo na kutatua changamoto zinazojitokeza na kuboresha zilizotatuliwa na kuongeza ubora zaidi.












Hakuna maoni:

Chapisha Maoni